Header Ads Widget

MAANDALIZI KUWASHWA MWENGE WA UHURU KITAIFA YAPAMBA MOTO PWANI..

 




Na Mwandishi wetu... MATUKIO daima.

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametembelea Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha utakapowashwa Mwenge wa Uhuru Kitaifa Aprili 2 Mwaka huu.


Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maandalizi yamefikia asilimia 96.


Kunenge amesema kuwa kwa sasa zimebaki siku sita ambapo Mwenge utazinduliwa Aprili 2 na utatembelea kwenye Halmashauri tisa za mkoa huo kwa kuanza na Halmashauri ya Mji Kibaha utakapoanzia.


"Uwanja umekamilika yamebaki maeneo machache ambapo hadi leo sehemu kubwa itakuwa imekamilika na kubaki mambo madogo madogo,"amesema Kunenge.


Amesema kuwa majukwaa yamekamilika na matarajio ni kuwa na watu 16,000 ambapo miundombinu ya maji, sehemu ya magari kukaa tayari, taa, mifumo ya majitaka na ulinzi viko tayari.


mwisho.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI