Header Ads Widget

TFS YACHANGIA UJENZI WA OFISI UWAMAKIZI




NA AMINA SAIDI,TANGA


Wakala  wa huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa kiasi cha sh.8,300,000 kwa ajili ya kuchangia ujenzi  wa ofisi ya Umoja wa  wakulima uhifadhi mazingira Kihuwi Zigi( UWAMAKIZI ),ujenzi wa ofisi ya mtendaji Mbambara na ofisi ya Elimu kata ya kisiwani zilizopo wilaayani Muheza Mkoani Tanga.



 Hayo aliyasema Mhifadhi  mkuu wa Misitu ,Shamba la miti Longuza Kata ya Amani walayani Muheza Erinema Masalanga wakati akikabidhi msaada wa mbao za kupaulia  kwa  UWAMAKIZI ikiwa ni moja ya mchango wa maendelea kwa jamii katika kazi za uhifadhi  unaofanywa kila mwaka .



Aidha alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 wamefanikiwa kutoa vifaa vya ujenzi kwa  taasisi mbalimbali ikiwemo ,UWAMAKIZI mbao za kupaulia zenye jumla ya thamani ya sh.3,888,000/=,ofisi ya mtendaji Mbambara mbao za kupaulia zenye thamani ya sh.1,340,000/=ofisi  ya idara ya elimu kata ya kisiwani mbao za Kupaulia zenye thamani ya sh.1,800,000/= na ofisi ya CCM-Kata ya Nkumba mifuko ya saruji yenye thamani ya


sh.672,000/=pamoja na gharama za usafirishaji wa vifaa hivyo ambayo ni sh.300,000/=inayofanya jumla kuu ya thamani sh.8,300,000.



Sambamba na hayo  Mhifadhi mkuu alitoa witoa kwa wananchi kuzingatia utunzaji wa Mazingira,kuheshimu mipaka ya maeneo ya hifadhi za misitu ikiwa ni pamoja na kuzuia uchimbaji wa madini  katika maeneo ya hifadhi hususan hifadhi za mito popote zilipo  pia kuwafichua wahalifu na kuchukua stahiki ili kulinda maeneo kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.



Kwa upande wake mwenyekiti wa UWAMAKIZI  Twaha Mbarouk  aliwashukuru na kuwapongeza  wakala wa huduma za Misitu Tanzania kupitia mhifadhi mkuu ,shamba la Longuza kwa kuwa na utaratibu wa kutoa mchango wa maendeleo kwa jamii zilizopo jirani na hifadhi .


 Naye Mkuu wa wilaya Muheza  Juma Irando ambaye alikuwa mgeni  rasmi katika shughuli hiyo  ya ugawaji wa vifaa vya ujenzi alitoa wito kwa wananchi na taifa kwa ujumla  kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake katika kuhakikisha rasilimali za  misitu na vyanzo vya Maji zinalindwa ili kunusuru mabadiliko ya tabia ya nchi na madhara yake.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI