Header Ads Widget

BREAKING:DKT KITIMA AJERUHIWA NA WATU WASIOJULIKANA

 



Hofu kubwa imetanda kufuatia tukio la kuvamiwa na kujeruhiwa kwa Katibu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania (TEC) Padri Dkt.Charles Kitima .

Kupitia mitandao ya kijamii imeripotiwa kuwa watu Wasiojulikana walimvamia Dkt Kitima majira ya saa 3 usiku April 30 mwaka huu na kuanza kumshambulia wakati  akiwa kwenye makazi yake yaliyopo  Ofisi za TEC Kurasini Dar Es salaam.


Mashuhuda wa tukio  hilo waliokuwa eneo la tukio lililozungukwa na mgahawa walisema  kuwa Padri Dkt Kitima ikiwa ni utamaduni wake wa kupita na kusalimu watu katika mgahawa mmoja eneo Hilo , ghafla walitokea watu Wasiojulikana na kuanza kumshambulia kwa sekunde chache na kisha kuondoka.

 Padri Kitima alijeruhiwa maeneo mbali mbali ya Mwili maana alikuwa  akivuja damu katika sehemu mbalimbali za mwili wake na haijulikani alijeruhiwa na kitu Gani.

Mara baada ya shambulizi hilo,Dkt Kitima amepatiwa matibabu ya awali kwenye Kituo kidogo cha afya cha TEC kilichopo eneo hilo .

TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUWALETEA BAADA YA KUMPATA KAMANDA WA POLISI  KWA UTHIBITISHO ZAIDI .


BOFYA LINK HII KUTAZAMA TAARIFA YA HABARI



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI