Header Ads Widget

DC ARUMERU AKAGUA UTEKELEZAJI MIRADI YA BOOST

 


Na,Jusline Marco ;Arusha



Mkuu wa Wilaya ya Arumeru  Mhe.Emmanuela  Kaganda  amesema Serikali  ya awamu ya sita  imejipanga kuwaletea wananchi wake maendeleo kwa ngazi zote.



Mhe.Kaganda wakati wa ziara yake ya kukagua utekezaji wa miradi ya BOOST katika Halmashauri  ya Wilaya ya Meru ambapo katika sekta ya elimu msingi,serikali imetoa shilingi milioni 961.5 fedha za BOOST kwa ajili ya  uboreshaji wa miundombinu katika shule za msingi ili kuhakikisha watoto wa Kitanzania  wanapata elimu bora katika mazingira rafiki.


Aidha Mhe.Kaganda ameelekeza miradi inayotekelezwa kuwa na viwango na ubora  unaotakiwa sambamba na kutekelezwa kwa wakati .




Awali akizungumza katika ziara hiyo Diwani  wa Kata ya Majengo Mhe.Bernard Kivondo amemshukuru  Rais.Dkt.Samia kwa kuendelea kutoa fedha za maendeleo katika  shule ya Msingi Kaloleni kwa awamu ambapo Serikali kupitia TASAF  ilitoa milioni 74 za ujenzi wa Vyumba viwili vya madarasa na ofisi.


Aidha Mhe.Kivondo ameongeza kuwa serikali pia ilitoa fedha shilingi milioni 12.5 za ukamilishaji wa boma na sasa imetoa  shilingi Milioni 106.3 fedha za mradi wa BOOST  kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitatu vya  madarasa  na vyoo .


Nao baadhi ya wananchi wa Kijjiji cha Kaloleni  Kata ya Majengo Halmashauri  ya Wilaya ya Meru,  Wilayani Arumeru wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu kwa kutoa fedha shilingi Milioni 106.3 za ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa  na vyoo vya  wanafunzi  wa kike matundu manne.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS