Header Ads Widget

MBARALI WAJA NA MKAKATI KUWABANA WANAOTELEKEZA WATOTO


Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbarali,Twalib Lubandamo

Na Matukio daima media, Mbarali

ASILIMIA kubwa ya utelekezaji wa watoto katika halmashauri ya wilaya

ya Mbarali mkoani Mbeya unatokana na unyanyasi wa wanaume kwa

wanawake  ambao hutokana na vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa

vikiendelea kufanywa  na kupelekea  kutekeleza familia zao .


Wilaya ya Mbarali imekuja na mwarobaini wa changamoto hiyo  ambapo

uongozi  uongozi wa halmashauri hiyo  umepanga kukabiliana na tatizo

hilo  kwa kutembea  kata , vitongoji ,vijiji kuangalia  kiini cha

tatizo hilo  na kupata suluhisho  na tatizo hilo kuisha  kabisa .


Hayo yammesemwa leo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Mbarali

mkoani Mbeya ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Itamboleo, Twalib

Lubandamo wakati wa kikao cha mkutano wa kawaida wa

baraza la madiwani wilayani  humo uliofanyika jana katika ukumbi wa

Maji.


Lubandamo amesema kuwa kero kubwa ambayo anakutano nazo  katika ofisi

yake ni ugomvi wa ndoa na familia  zilizotelekezwa  na kusema mpaka

sasa analea familia sita zilizotelekezwa .


‘’Nina mtoto mwingine ambaye nimemchukua  Igurusi Sekondari yupo

vizuri sana kimasomo ambaye amepata ufaulu mzuri sana  kwenye  matokeo

yake ya kidato cha Nne ,ninao watoto wengi ninaolea sisi wanaume

tumekuwa wanyanyasi wakubwa kwa wanawake  hivyo wanawake wanaenda

kupata shida na watoto  kwa hiyo kero nyingi tulizo nazo asilimia

kubwa ni wanawake  kuja na familia zao na ugomvi wa ndoa  unakuta muda

mwingine mwanamke anakuja kapigwa mpaka katolewa sikio kung’atwa ulimi

 kwakweli wanaume tumekuwa wakatili sana ,wiki iliyopita alikuja Mama

mmoja na watoto sita hawajala chochote hivyo ilibidi kama halmashauri

tujichange kumsaidia mama huyu ‘’amesema Mwenyekiti huyo wa

halmashauri .


Akizungumzia zaidi Mwenyekiti huyo amesema  kama halmashauri

wamejipanga  kwa kukabiliana kuwa kila kijiji , kitongoji kuanzia

Mwezi marchi kwenda kuangalia changamoto za wanawake na kuhakikisha

zinakwisha moja kwa moja.


Kaimu Mganga mkuu Halmashauri ya wilaya ya Mbarali idara ya afya na

ustawi wa jamii na lishe , Dkt.Ray salandi amesema  kuwa kitengo cha

ustawi wa jamii kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha walikuwa na jumla

ya migogoro ya kifamilia  334 ambapo  kwa asilimia kubwa migogoro

hiyo imetokana na ukatili wa kimwili  kwa maana ya  vipigo  ambavyo

vinafanya  jumla ya vipigo 113 ambayo ni sawa na asilimia 34

iliyosuruhishwa kwa kipindi cha  robo ya pili.


Hata hivyo Dkt.  Salandi amesema changamoto nyingine kubwa  ni matunzo

kwa watoto ambapo kulikuwa na familia 106, zilikuwa na changamoto ya

matunzo kwa watoto  na kufan ya kufanya asilimia 32 hivyo kwenye

idara hiyo wameendelea kutatua changamoto  na migogoro 334 ,ilifika

kikomo kwa kufuata taratibu za kisheria  ikiwemo polisi.


Diwani wa Kata ya Miyomboni ,Jeremiah Kisangai amesema utelekezaji

watoto unasabishwa  na wanaume kuingia kwenye mahusiano na kusabisha

mimba zisizotarajiwa  kwa asilimia kubwa kama halmashauri  zoezi

lilishafanyika la kuwapitia  na kupatikana kwa mashauri  mengi zaidi

ya 300.


Kisangai amesema kuwa  baada ya kuyapitia walibaini vitu vingi  lakini

kubwa halmashauri imejipanga kwenye maeneo ya vijiji kuna kamati

zinazoshughulikia kukaa kila wakati kushughulikia kero hizo ili

kupunguza matatizo hayo hususani Madiwani .


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI