Header Ads Widget

UWT MKOA WA IRINGA WAVUTIWA NA UTENDAJI WA RAIS DKT SAMIA WAJIPANGA KUMCHUKULIA FOMU YA URAIA TENA

 


UMOJA wa wanawake Tanzania (UWT) mkoani Iringa umesema kutokana na uongozi bora ulionyeshwa na serikali ya awamu ya sita pamoja na utekelezwaji mzuri wa Ilani ya chama hicho kwa pamoja umeamua kuwa utamchukulia fomu ya kugombea Urais 2025, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili kuweza kukamilisha yale yote ambayo yatakuwayamesalia katika kuwatumikia Watanzania.



Hayo yamesemwa na katibu wa CCM mkoa wa Iringa, Rukia Mkindu ambayealimwakilisha wa mgeni rasmi MNEC Salim Abri Asas  katika kikao Cha baraza kuu la UWT mkoa wa Iringa lililofanyika Ukumbi wa CCM mkoa .

"Katika kuhakikisha kuwa yale alitoyaanzisha Mama yetu mpendwa Mama

Samia yanakamilika, sisi kama CCM Iringa tumejipanga kumchukulia fomu

ya ugombea Urais na kuigharamia kwa 100%..." Alisema.

Asas alimewataka akina mama wa mkoa wa Iringa kuitumia mikopo inayotolewa na serikali

ya awamu ya sita ili iwasaidie kuwainua kiuchumi kwani ni kwa ajili

yao.


"Mikopo inayotolewa na awamu ya sita ni kwa ajili yetu akina mama,

tuitumie kutunufaisha na kutuinua kiuchumi. Bahati nzuri mikopo ya

kipindi hiki sio mikopo kiduchu, ni mikopo ya kututoa kwenye wimbi la

umaskini kama tutaitumia vizuri"


Awali akifungua kikao hicho mwenyekiti wa umoja wa wanawake mkoa wa

Iringa Zainabu Mwamwindi amewataka kushikimana kwa pamoja katika

kipindi hiki ambacho uchaguzi umekwisha ili kuweza kuwatumikia

wananchi kwa ngazi zote.


"...Katika kipindi hiki ambacho hatuna uchaguzi na tunajiandaa kwa

chaguzi zijazo, ni wakati wa sisi kukijenga chama chetu katika nyanja

zote kupitia jumuiya zetu za wazazi, wanawake na vijana ili tufanye

vizuri katika uchaguzi ujao.


Mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego alisema umoja wa wanawake

Tanzania (UWT) unakuwa kioo kwa wanawake wengine ambao wapo nje ya

umoja huo pamoja kuwasaidia katika kutatua changamoto zao kwa

kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI