JESHI la polisi mkoa wa Iringa linamshilia watuhumiwa 10 akiwemo wakala wa kampuni ya Selcom Paytech Limited kijana Tyason Kasisi ambaye alikuwa akitoa huduma ya Selcom Pay kwa wizi wa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 2,129,856,000 mali ya kampuni ya Selcom Paytech Limited .
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Allan Bukumbi aliwaeleza waandishi wa habari kuwa mtuhumiwa huyo kupitia huduma ya Selcom pay isiyo haliali alihamisha fedha kwenda kwenye namba mbali mbali za simu na kisha kuchukuliwa taslimu kupitia wakala wa huduma za kifedha za mtandao mbali mbali ya simu pamoja na akaunti za Benk.
“ wizi wa fedha hizo ulifanyika kwa njia ya mtandao katika mkoa wa Iringa ,Dar es Salaam na Morogoro kati ya tarehe 9 hadi tarehe 27 Novemba 2021 baada ya wakala huyo Tyason Kasisi kufanikiwa kuchezea mfumo wa kieletroniki wa “Selcom Pay’ unaomilikiwa na kampuni ya Selcom Paytech Limited” alisema kamanda Bukumbi
Kuwa wakala huyo kwa njia ya udanganyifu alianza kujitumia fedha pamoja na kuwatumia watu wengine na kwa kushirikiana na genge la uhalifu walifanikiwa kuiba kiasi hicho cha Tsh 2,129,856,000
Hata hivyo alisema jeshi la polisi limefanikiwa kukamata (kuokota) fedha kiasi cha shilingi 956,974,000 kutoka kwa watuhumiwa na washirika wa uhalifu huo ambao walipokea sehemu ya fedha hizo kwa njia ya kuzificha katika maeneo mbali mbali ikiwemo makazi na shambani pia kiasi cha fedha shilingi 121,215,783 zimezuiliwa katika moja ya benk za kibiashara mkoa wa Iringa ikiwa ni mali ya uhalifu .
Alisema kuwa upelelezi uliofanywa hadi sasa umebaini kuwa genge hilo la uhalifu na wizi wa fedha za kampuni hiyo uliongozwa na watu watatu ambao ni Tyson Kasisi ,Patrick Chalamila na Evaristo Chalamila ambao wamebaikika kuwa ni wanufaika wakuu wa uhalifu huo .
Aidha alisema mbali ya fedha hizo kukamatwa pia mali zinazosadikika kuwa za uhalifu huo zimekamatwa na kuhifadhiwa ikiwa ni pamoja na magari manne yenye thamani ya Tsh 303,000,000 .
Kamanda Bukumbi alitaja mali hizo kuwa ni Scania yenye jina la mtuhumiwa Patrick Chalamila lenye thamani ya shilingi milioni 128, Mitsubish Fuso yenye usajili namba T 796 DXV yenye jina la mtuhumiwa Tyson Kasisi likiwa ni thamani ya shilingi milioni 75, gari aina ya Toyota Harrier lenye usajili T 719 DXX lenye jina la Tyson Kasisi likiwa na thamani ya shilingi milioni 72 na gari aina ya Nissan Juke lenye usajili T 605 DXV lenye jina la Patrick Chalamila likiwa na thamani ya shilingi milioni 28.
Pia jeshi la polisi limekamata gari aina ya Toyota IST yenye namba za usajili T 576 DRN mali ya Patrick Chalamila lililotumika kufanikishia uhalifu kwa kusafirisha fedha hizo za wizi kutoka Madibila wilayani Mbarali ,Ilula wilaya ya Kilolo kwenda kuzificha Kilombero mkoani Morogoro.
Kamanda huyo alisema kuwa ushahidi uliokusanywa hadi sasa umetosha kuwafikisha watuhumiwa 10 mhakamanani kujibu tuhuma zinazowakabili za kuongoza genge la uhalifu pamoja na kujipajia fedha kwa njia ya udanganyifu .
0 Comments