Header Ads Widget

HUDUMA ZA MAKTABA KUPATIKA KWA NJIA ZA KIDIGITALI

Prof. Frankwell  akizungumza na wanahabari 

Maktaba ya mkoa wa Iringa 

Na Rehema Abraham Kilimanjaro

Wadau wa maktaba nchini wamekutana mkoani Kilimanjaro katika kongamano la kisayansi la shirikisho la vyuo vikuu na vyuo vya utafiti kujadili namna Bora ya kuboresha na namna  ya upatikanaji wa huduma za maktaba na utumiaji wake katika njia ya kidigitali.

Akizungumza katika warsha hiyo Naibu makamu Mkuu wa chuo kikuu Cha ushirika Moshi  prof. John Safari amesema warsha hiyo itakwenda kusaidia wanaofanya kazi za maktaba Kama waalimu na na wafunzi wataweza kupata taarifa hizo kwa usahihi.


Kaimu Makamu Mkuu wa chuo kikuu Cha ushirika Moshi profesa John Safari

Amesema kuwa watahakikisha kuwa waalimu na wanafunzi waliopo kwenye nafasi za elimu ngazi ya juu  wanatumia makala na maandiko za kitaaluma zilizopo kwenye mfumo wa kidigitali. 


"Kwenye upande wa uchapishaji na tafiti mbalimbali taasisi zetu hazijawaa kwenye ngazi Nzuri sana ya kidunia hivyo ninawataka watu wa Tasisi zote za elimu ya juu kufanya jitihada zaidi ya kuhakikisha kuwa wanafanya matangazo kwenye majarida ambayo yanakubalika kidunia ili tuweze kutambulika kidunia kuwa vyuo vikuu  vya Tanzania zina sifa Kama vyuo vingine vya Afrika mashariki"Alisema Safari.



Aidha mwenyekiti wa shirikisho Hilo Prof. Frankwell Dule amesema kuwa kongamano Hilo litawajengea uwezo wa kuandika tafiti za kitaaluma na kuwafikia walengwa.


Kwa upande wake Grece msofe mkurugenzi wa huduma za maktaba kutoka Dodoma  amesema kuwa machapisho ambayo yapo kwenye njia ya makaratasi na hayawezi kupatikana mtandaoni kompyuta au simu kwa sasa Wana uwezo wa kuchapisha hayo machapisho na kuweka ili kusomeka kwa kutumia dhana mbalimbali za kielektronick.


Hata hivyo Dr Visent Msonge  katibu Mkuu wa ( COTUL)shirikisho la maktaba  ya vyuo na vyuo vya na vyuo vya utafiti ,na mkurugenzi wa huduma za maktaba katika chuo Cha usimamizi wa fedha amesema kuwa warsha hiyo imelenga kuonesha jukumu la maktaba katika kuwasaidia  watafiti nchini kuwa katika ulimwengu wa kidigitali .


"Imekuwa ni changamoto kubwa ndani ya tasisi zetu hasa hapa Tanzania kuonekana machapisho ,kwa hiyo lengo letu kubwa la kufanya haya makongamano Kama hayo ili taarifa zinaweza kuwafikia walengwa "Alisema Msonge.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI