Na Teddy Kilanga,MDTV Arusha
Serikali ya Tanzania na Kenya imeendelea kujadili na kuweka makubaliano ambayo yatasaidia kukamilisha mikataba inayotarajiwa kusahiniwa hivi karibuni kati ya nchi hizo ambapo matokeo yake kuongeza ushirikiano.
Akizungumza na waandishi wa habari kando ya mkutano wa watalam,Afisa Mwandamizi kutoka wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki ,Paul Makelele alisema lengo la mkutano huo ni kutokana na maelekezo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya katika kujadili mikataba uliofanyika Nairobi mnamo Agasti 20 hadi 24 Mwaka huu
Alisema kupitia mkutano huo ilielekezwa kwamba kuna baadhi ya mikataba ambayo haijakamilika katika hutiaji wa saini kati ya nchi hizo mbili hivyo ilielekezwa kwamba timu za wataalamu kati ya Tanzania na Kenya wakutane nchini Tanzania kwa ajili ya kukamilisha majadiliano ya mikataba hiyo na ikiwezekana isahiniwe kwa miezi michache inayokuja.
"Mikataba ambayo inajadiliwa ni pamoja na makubaliano ya masuala ya uhamiaji,mkataba wa kuhusu masuala ya kupeana wahalifu,kusaidiana katika makosa ya jinai,mabadilisho ya wafungwa kati ya nchi hizo,hati ya makubaliano ya kuhusu masuala ya magereza pamoja na uwekezaji,"alisema Makelele.
Aidha alisema wanatarajia kwamba majadiliano hayo yatadumu kwa siku tano yatakamilisha makubaliano ya mikataba hiyo ili iweze kusainiwa kwa miezi michache inayokuja ikiwa katika mkutano huo umewashirikisha wataalamu kutoka uhamiaji,magereza,wizara ya katiba na sheria,Ofisi ya Mwanasheria mkuu wa serilikali na wizara ya mambo ya nje.
Hata hivyo alisema mkutano huo wa wataalamu umefunguliwa na balozi wa Tanzania nchini Kenya,George Simbachawene pamoja na balozi wa Kenya nchini Tanzania Dan kazungu unaotarajiwa kufungwa mnamo Novemba 12,2021.





0 Comments