Header Ads Widget

CBS YACHAPISHA PICHA ZA UHARIBIFU KATIKA KAMBI ZA MAREKANI


 Mtandao wa habari wa Marekani, CBS, ambao ni mshirika wa BBC nchini humo, umechapisha kwa mara ya kwanza picha mpya zinazoonyesha kile unachosema ni uharibifu mkubwa uliosababishwa na mashambulizi ya Iran dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa CBS, picha hizo za kipekee zinaonyesha uharibifu mkubwa katika baadhi ya kambi za kijeshi za Marekani, ambapo majengo, magari ya kijeshi na miundombinu mingine iliharibiwa katika mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani.


Mmoja wa wanajeshi walioko katika kambi hizo alinukuliwa na CBS akisema kuwa ukubwa wa uharibifu uliosababishwa na mashambulizi hayo haujawekwa wazi kikamilifu kwa umma wa Marekani.

"Hii ni hasara kubwa kwa kambi zetu ambayo wananchi wa Marekani hawajafahamishwa kikamilifu. Tumekuwa tukikabili mashambulizi mfululizo huku tukionekana kutokuwa na uwezo wa kujibu kwa ufanisi," alisema.


Miongoni mwa picha zilizosambazwa ni moja inayodaiwa kupigwa katika Kambi ya Jeshi la Anga ya Prince Sultan nchini Saudi Arabia. Picha hiyo inaonyesha kile kinachodaiwa kuwa athari ya shambulio la moja kwa moja kwenye sehemu ya nyuma ya ndege ya kijeshi ya Boeing A-3 Sentry yenye injini nne.

Katika picha hiyo, mkia wa ndege unaonekana kuwa umetenganishwa na sehemu kuu ya mwili wa ndege, huku mabaki yake yakionyesha dalili za kuungua. Uharibifu pia unaonekana kuathiri sehemu iliyobeba mfumo wa rada unaozunguka, unaotumiwa kufuatilia na kukusanya taarifa kuhusu shughuli za angani.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI