Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza rasmi matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne (CSEE) 2025 leo Januari 31, 2026, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Tangazo hilo limetolewa na Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said Mohammed, ambapo ameeleza kwa kina hali ya ufaulu na ushiriki wa watahiniwa nchini kote.
👉 BOFYA HAPA KUTAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2025 (NECTA)
👉 MATOKEO YA CSEE 2025 – NECTA
Taarifa Muhimu Kuhusu Matokeo ya Kidato cha Nne 2025
Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2025 ulifanyika kuanzia Novemba 17, 2025, ukihusisha:
-
Watahiniwa 569,883 kutoka shule 5,864
-
Watahiniwa wa kujitegemea 25,927
-
Mahudhurio ya jumla: asilimia 97.5
NECTA imeeleza kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.61, na kufikia asilimia 94.98, ambapo jumla ya watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata daraja la kwanza hadi la nne.
Ufaulu Waongezeka – Ubora wa Elimu Waendelea Kuimarika
Kwa mujibu wa NECTA:
-
Watahiniwa 255,404 sawa na asilimia 46.1 wamepata daraja la kwanza hadi la tatu
-
Hali hii inaonesha kuimarika kwa ubora wa elimu ya sekondari nchini Tanzania
Jinsi ya Kuangalia Matokeo ya Kidato cha Nne 2025 NECTA
-
Tembelea tovuti rasmi ya NECTA
-
Chagua Matokeo ya CSEE 2025
-
Ingiza namba ya mtihani
-
Bonyeza Tazama Matokeo






0 Comments