Header Ads Widget

WAZIRI WA ULINZI PETE HEGSETH AMTAKA MKUU WA MAJESHI KUACHIA NGAZI

 

Mkuu wa Jeshi la Marekani Randy George

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth amemtaka Mkuu wa Majeshi Randy George kuachia wadhifa wake, kulingana na CBS News, mshirika wa habari BBC wa Marekani.

Msemaji Mkuu wa Pentagon Sean Parnell alisema katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii kwamba George "atastaafu kutoka wadhifa wake kama Mkuu wa 41 wa Wanajeshi mara moja".

Mkuu wa Jeshi kawaida huhudumu kwa kipindi cha miaka minne.

George, afisa wa kijeshi ambaye alihitimu kutoka chuo cha kijeshi cha West Point, aliteuliwa kwa jukumu hilo mnamo 2023 na Rais wa zamani Joe Biden.

Mabadiliko ya hivi punde yanakuja baada ya Trump kusema katika hotuba yake kwa taifa kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinatarajiwa kumalizika "hivi karibuni".

George aliwahi kuwa afisa wa jeshi katika Vita vya kwanza vya Ghuba na katika migogoro ya hivi majuzi nchini Iraq na Afghanistan.

Haijabainika kwa nini alitakiwa kuondoka. "Tunashukuru kwa utumishi wake, lakini ulikuwa wakati wa mabadiliko ya uongozi katika Jeshi," afisa mkuu wa ulinzi ambaye hakutajwa jina aliiambia CBS.

Msemaji wa Pentagon Parnell alisema: "Idara ya Vita inashukuru kwa miongo kadhaa ya utumishi wa Jenerali George kwa taifa letu. Tunamtakia kila la heri anapostaafu."

Nafasi yake itachukuliwa na Makamu Mkuu wa Jeshi Jenerali Christopher LaNeve ambaye atakuwa kaimu mkuu wa majeshi, kulingana na vyombo vya habari vya Marekani.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI