Baada ya kushambuliwa na ndege zisizo na rubani nyingi asubuhi ya Ijumaa, moto ulizuka katika sehemu za kiwanda muhimu cha kusafisha mafuta huko Kuwait.
Hakuna majeraha walioripotiwa.
Kiwanda cha kusafisha mafuta cha Mina al-Ahmadi, ambacho ni mojawapo ya vikubwa zaidi Mashariki ya Kati, kinaweza kusafisha hadi mapipa 346,000 ya mafuta kwa siku.
Kuwait ina viwanda vitatu vikubwa vya kusafisha mafuta. Kiwanda chake cha kusafisha mafuta cha Mina al-Ahmadi kimekuwa kikilengwa na ndege zisizo na rubani za Iran mara mbili hapo awali wakati wa mzozo wa wiki tano.
Shirika la Petroli la Kuwait linasema timu za dharura na zimamoto zimekuwa zikifanya kazi ya kudhibiti moto katika baadhi ya vitengo 39 vya kiwanda cha kusafishia mafuta na kuzuia kuenea kwake.
Inaongeza kuwa ubora wa hewa katika eneo lililoathiriwa unafuatiliwa, na kwamba hadi sasa hakuna athari yoyote kwenye mazingira ya eneo hilo.
Maafisa wanasema Iran yashambulia kiwanda cha kuondoa chumvi kwenye maji Kuwait
Wizara ya Umeme na Maji ya Kuwait imesema kiwanda cha kuondoa chumvi kwenye maji kimeshambuliwa na Iran, na kusababisha "uharibifu wa vifaa".
Timu za kiufundi na za dharura zilianza kazi "mara moja" ili "kudumisha ufanisi wa uendeshaji", inasema katika taarifa kwenye mtandao wa X.
"Usalama na uthabiti wa mfumo wa umeme na maji ni kipaumbele cha juu," taarifa hiyo inaongeza.





0 Comments