Donald Trump amemkosoa vikali Papa Leo XIV kwenye mitandao ya kijamii baada ya kiongozi wa kwanza wa Marekani wa Kanisa Katoliki Duniani kulaani tishio la rais wa Marekani dhidi ya Iran.
Katika chapisho refu kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, rais huyo wa Marekani aliandi Papa "ni mbaya kwa Sera ya Kigeni".
"Simtaki Papa ambaye anadhani ni sawa kwa Iran kuwa na Silaha ya Nyuklia," Trump alisema.
Akiorodhesha malalamiko mengine dhidi ya Papa, Trump aliandika kwamba Papa Leo ni "Weak on Crime, Weak on Nuclear Weapons".
Akiorodhesha malalamiko mengine dhidi ya Papa, Trump aliandika kwamba Papa ''hana nguvu kushughulikia uhalifu na silaha za nyuklia''.
Wiki iliyopita, Papa Leo alikosoa tishio la Trump kwamba "ataiangamiza Iran usiku wa leo" nchi hiyo isipofikia makubaliano ya kumaliza vita.
Akisisitiza kuwa tamko kama hilo "halikubaliki", Papa aliongeza kusema: "Kuna maswali ya sheria ya kimataifa, lakini zaidi ya yote, ni suala la kimaadili."
MWISHO.





0 Comments