Peter Magyar ameshinda uchaguzi mkuu wa Hungary,huku chama chake kikipata theluthi mbili ya viti vya ubunge katika uchaguzi ambao unamuondoa madarakani Waziri Mkuu Victor Orban aliyeliongoza taifa hilo kwa miaka 16.
Bwana Magyar ameuambia umati mkubwa wa wafuasi mjini Budapest kuwa Hungary inataka tena kuwa taifa la Ulaya na kuongeza kuwa wamefanikiwa kuleta muujiza katika historia ya Hungary kwa kushinda uchaguzi huo kwa kishindo.
Waziri Mkuu huyo ajaye wa Hungary ameahidi kipindi cha kukabidhiana madaraka kitakuwa cha amani.Viongozi kadhaa wa nchi za Umoja wa Ulaya wamempongeza Magyar kwa ushindi huo.





0 Comments