Header Ads Widget

KIONGOZI WA KIJESHI WA BURKINA FASO LAZIMA 'ISAHAU' KUHUSU DEMOKRASIA

 

Demokrasia "inaua" na watu wa Burkina Faso lazima "wasahau" hili, Rais wa kijeshi wa nchi hiyo amesema katika mahojiano yaliyorushwa hewani kwenye televisheni ya serikali.

Kapteni Ibrahim Traoré, ambaye alichukua madaraka katika mapinduzi ya kijeshi miaka mitatu iliyopita, alisemaa kwamba Waafrika wengi hawataki mfumo wa demokrasia na kwamba Burkina Faso ilikuwa na mbinu yake mbadala, bila kutoa maelezo zaidi.

Awali, Traoré aliahidi kurejesha utawala wa kidemokrasia katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi ifikapo Julai 2024, lakini miezi miwili kabla ya tarehe hii ya mwisho, utawala wa kijeshi ulitangaza kwamba utaongeza utawala wake kwa miaka mingine mitano.

Miezi miwili iliyopita, mamlaka zilitangaza kupiga marufuku vyama vyote vya siasa kama sehemu ya mpango wa "kujenga upya taifa hilo".

Katika mahojiano ya Alhamisi usiku, Traoré alisema: "Watu wanahitaji kusahau kuhusu suala la demokrasia. Demokrasia si yetu."

"Tazama Libya, huu ni mfano unaotukaribia," alisema rais huyo mwenye umri wa miaka 38.

Libya ilitawaliwa kidemokrasia kwa miongo minne na Kanali Muammar Gaddafi, ambaye alisimamia utawala wa ukatili huku pia akiwapa Walibya ruzuku ya makazi, elimu ya bure na huduma ya afya ya bure.

Aliuawa wakati wa uasi uliosaidiwa na uingiliaji kati wa kijeshi wa Magharibi. Tangu wakati huo, nchi hiyo ya Afrika Kaskazini imeshindwa katika dhamira yake ya kuanzisha demokrasia na badala yake imegawanyika kati ya tawala mbili hasimu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI