Mahakama ya Kenya jana Jumanne ilimshtaki mwanamume mmoja kwa biashara ya pembe mbili za faru zenye thamani ya shilingi milioni 8.2 za Kenya (dola 63,000), miaka tisa baada ya kufungwa jela kwa kusafirisha pembe za ndovu.
Feisal Mohamed Ali na mshukiwa mwenzake Mohammed Hassan walikamatwa katika mji wa bandari wa Mombasa mwezi uliopita.
Siku ya Jumanne, wawili hao walikana shtaka la kuhusika na wanyamapori walio hatarini kutoweka.
Ali aliachiliwa baada ya kukata rufaa mwaka wa 2018, miaka miwili ndani ya kipindi cha miaka 20 alichohukumiwa kwa ulanguzi wa pembe za ndovu, kutokana na dosari za utaratibu katika kesi hiyo.
Polisi walikuwa wamemshutumu kwa kuhusika na kundi la kimataifa la uwindaji haramu lililohusishwa na kunaswa kwa meno 120 ya ndovu.
0 Comments