Header Ads Widget

IRAN YAMHUKUMU KUNYONGWA MTU ANAYETUHUMIWA KUFANYA UJASUSI WA ISRAEL

Iran imemhukumu kunyongwa mtu aliyetuhumiwa kufanya ujasusi kwa ajili ya Israel, kulingana na ripoti kutoka kwa vyombo vya habari vya serikali siku ya Jumatano aliyetambulishwa kama Babak Shahbazi.

Iran imetoa hukumu ya kifo kwa watu wengi inaowatuhumu kuwa na uhusiano na idara ya kijasusi ya Israel ya Mossad na kuwezesha shughuli zake nchini humo.

Visa vya hukumu ya kunyongwa kwa Wairani waliopatikana na hatia ya kufanya ujasusi kwa ajili ya Israel vimeongezeka kwa kiasi kikubwa mwaka huu, huku takriban hukumu tisa za vifo zikitekelezwa katika miezi ya hivi karibuni.

Vyombo vya habari vya serikali vilisema Shahbazi alifanya kazi na Esmaeil Fekri, mfungwa mwingine aliyenyongwa mwezi Juni kwa kufanya ujasusi wa Israel tangu mapema 2022.

Shahbazi alishtakiwa kwa kutumia wadhifa wake kama mwanakandarasi anayeweka vifaa vya kupozea ili kukusanya taarifa kutoka sehemu nyeti na vituo vinavyohusishwa na jeshi na vyombo vya usalama.

Wakili wa mshtakiwa alikuwa ameomba kukata rufaa kwa Mahakama ya Juu Zaidi, ambayo ilikataa ombi hilo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI