Rais Volodymyr Zelensky alishirikisha umma picha za wanajeshi wakisherehekea waliporejea Ukraine
Mabadilishano ya wafungwa yanaendelea kati ya Urusi na Ukraine, serikali za Moscow na Kyiv zimethibitisha.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema mazungumzo hayo yatafanyika "katika hatua kadhaa" katika siku zijazo, akiongeza kuwa waliojeruhiwa, waliojeruhiwa vibaya na wanajeshi walio chini ya miaka 25 wanarudishwa.
Akiandika kwenye Telegram, Zelensky alisema: "Mchakato huo ni mgumu sana, kuna maelezo mengi nyeti, mazungumzo yanayoendelea karibu kila siku."
Urusi ilisema "idadi sawa" ya wafungwa wa kivita wamerudishwa Ukraine, ingawa hakuna upande uliotoa takwimu kamili ya ni watu wangapi walibadilishwa.
0 Comments