Marufuku mpya ya kusafiri ya Rais Donald Trump ambayo inazuia raia wa nchi 12 kuingia Marekani ilianza kutekelezwa saa 00:00 ET (05:00 BST) Jumatatu.
Agizo hilo ambalo Trump alitia saini wiki iliyopita, linawazuia raia wa Afghanistan, Myanmar, Chad, Congo-Brazzaville, Equatorial Guinea, Eritrea, Haiti, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen kuingia Marekani.
Raia kutoka nchi saba zaidi - Burundi, Cuba, Laos, Sierra Leone, Togo, Turkmenistan na Venezuela - watakabiliwa na vikwazo vya kusafiri.
Rais wa Marekani alisema orodha hiyo inaweza kurekebishwa ikiwa "maboresho ya nyenzo" yatafanywa, wakati nchi nyingine zinaweza kuongezwa iwapo"vitisho vitatokea kote duniani".
Ni mara ya pili kwa Trump kuamuru marufuku ya kusafiri kutoka nchi fulani. Alitia saini agizo kama hilo mnamo 2017 wakati wa muhula wake wa kwanza ofisini.
Ikulu ya White House ilisema "vizuizi hivyo " "vitalinda Wamarekani kutoka kwa wahalifu wa kigeni".
Katika video iliyotumwa kwenye tovuti yake ya Mtandao wa Truth and Social wiki jana, Trump alisema shambulio la hivi majuzi huko Boulder, Colorado "lilidhihirisha hatari kubwa" inayoletwa na raia wa kigeni ambao "hawajachunguzwa ipasavyo".
Watu 12 walijeruhiwa huko Colorado tarehe 1 Juni wakati mtu mmoja aliposhambulia kundi lililokuwa likiunga mkono mateka wa Israel.
FBI ililitaja hilo kuwa shambulizi linaloshukiwa kuwa la kigaidi na kusema kwamba mshukiwa alitumia kifaa cha kuwasha moto, vinywaji vya Molotov na vifaa vingine vya kuwasha.
0 Comments