Header Ads Widget

ASHTAKIWA KWA MADAI YA KUMTILIA MPENZI WAKE DAWA YA KUTOA MIMBA

 

Mwanamume mmoja huko Texas ameshtakiwa kwa mauaji baada ya kudaiwa kuingiza dawa ya kutoa mimba kwenye kinywaji cha mpenzi wake mjamzito.

Justin Anthony Banta alikamatwa siku ya Ijumaa baada ya uchunguzi wa miezi kadhaa kuhusu tuhuma za mpenzi wake wa zamani kwamba alimpa tembe ya Plan C (inayojulikana kama dawa ya kutoa mimba) bila yeye kujua, kulingana na polisi katika jimbo la Marekani.

Mpenzi wa zamani wa Bw Banta alisema alipofichua ujauzito wake mwaka jana, alijitolea kulipia gharama ya kuavya mimba, lakini alionyesha nia yake ya kulea mtoto wake.

Polisi walisema baada ya kukutana na Bw Banta katika mgahawa mmoja, alipata damu nyingi na kupelekwa katika chumba cha huduma za dharura, lakini akampoteza mtoto wake siku chache baadaye.

Polisi walisema mpenzi wa zamani wa Bwana Banta alikuwa na ujauzito wa takriban wiki sita alipoenda kwa daktari wake, ambaye alimwambia mtoto alikuwa mwenye afya njema na "mapigo ya moyo" stahiki.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI