Mahakama ya Korea Kusini imemtoza faini mwanamke mmoja kwa kosa la utovu wa nidhamu baada ya kumvua suruali mwenzake wa kiume – na kwa bahati mbaya, pia nguo yake ya ndani ikavuka mbele ya wenzao, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.
Mbali na faini ya milioni 2.8 aliyotozwa ($2,100; £1,500), mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 pia ameamriwa kufanya mafunzo ya elimu ya kuzuia unyanyasaji wa kingono ya saa nane.
Kisa hicho kinaripotiwa kutokea Oktoba mwaka jana katika mgahawa mmoja jimbo la Gangwon kaskazini-mashariki.
Uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Chuncheon siku ya Jumamosi ulikataa madai ya mwanamke huyo kwamba alikusudia kufanya mzaha kwa mwenzake, ambaye yuko katika umri wa miaka 20.
0 Comments