Urusi inasema Ukraine imeanzisha shambulizi la usiku wa kuamkia jana na ndege isiyo na rubani iliyolenga Moscow kwa usiku wa pili mfululizo.
Viwanja vyote vinne vya ndege vikubwa vya mji mkuu vimefungwa kwa muda ili kuhakikisha usalama, shirika la uangalizi wa anga la Urusi Rosaviatsia lilisema kwenye Telegram.
Meya wa Moscow, Sergei Sobyanin, alisema kwenye mitandao ya kijamii takribani ndege 19 zisizo na rubani za Ukraine ziliharibiwa kabla ya kufika mjini "kutoka pande tofauti". Alisema baadhi ya vifusi hivyo vimetua kwenye moja ya barabara kuu za kuingia mjini, lakini hakuna majeruhi.
Ukraine bado haijasema chochote. Lakini meya wa Kharkiv alisema Urusi pia imefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika mji huo usiku kucha, na pia katika eneo la Kyiv.
Pamoja na huko Moscow, magavana wa miji mingine ya Urusi, pamoja na Penza na Voronezh, pia walisema walikuwa wakilengwa na ndege zisizo na rubani usiku wa Jumanne.
Ni usiku wa pili mfululizo ambapo Urusi imeripoti shambulio la ndege zisizo na siku ya Jumatatu, wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema kuwa imeharibu ndege 26 za Ukraine usiku kucha.
Tangu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine zaidi ya miaka mitatu iliyopita, Kyiv imeanzisha mashambulizi kadhaa ya ndege zisizo na rubani mjini Moscow. Shambulio lake kubwa zaidi mwezi Machi liliua watu watatu.
0 Comments