Gari la Papa Francis kubadilishwa kuwa zahanati
Moja ya magari yaliyotumiwa na Papa Francis kusalimia maelfu ya watu litageuzwa kuwa zahanati inayotembea ili kusaidia watoto wa Gaza.
Shirika la hisani la Caritas linalosimamia mradi huo, lilisema gari hilo lililotumika wakati wa ziara ya marehemu Papa mjini Bethlehem mwaka 2014, kwa sasa lina vifaa vya kutosha i kutoa huduma za afya katika maeneo ya vita, kwa ombi la Papa Francis.
Shirika hilo lilisema katika taarifa yake: "zahanati hiyo itakuwa na vifaa vya kufanya vipimo vya haraka, sindano, mitungi ya oksijeni, chanjo, na friji ndogo ya kuhifadhi dawa."
Vatican ilisema kuwa hilo lilikuwa ombi la mwisho la Papa kwa watoto wa Gaza kabla ya kifo chake mwezi uliopita.
Gari hilo kwa sasa liko Bethlehem na litaingia katika Ukanda wa Gaza wakatinjia ya kibinadamu itafunguliwa na Israel.
0 Comments