Header Ads Widget

ISRAEL YASHAMBULIA MAENEO YA WAHOUTHI NCHINI YEMEN

 

Jeshi la Israel linasema kuwa limeshambulia maeneo ya Wahouthi nchini Yemen kujibu kurusha kombora la kundi hilo katika uwanja wa ndege wa Ben Gurion siku iliyotangulia.

IDF ilisema ilishambulia maeneo ambayo ilidai kuwa "chanzo kikuu cha usambazaji wa Houthi" katika Bandari ya Hudaydah, pamoja na kiwanda cha saruji cha Bajil mashariki mwa jiji la Hudaydah.

Kufuatia shambulizi kwenye uwanja wa ndege Jumapili, Houthi walisema wataweka "vizuizi kamili vya anga" kwa Israel kwa kulenga viwanja vya ndege kujibu mipango ya Israel ya kupanua shughuli zao huko Gaza.

Kundi linaloungwa mkono na Iran limesema watu 21 walijeruhiwa katika shambulio hilo la Jumatatu, na kueleza kuwa ni uvamizi wa pamoja wa "uchokozi wa Marekani na Israel".

Marekani ilikana kuhusika. IDF ilisema shambulizi lake la Jumatatu "lilifanywa kwa usahihi, na hatua zilizochukuliwa kupunguza madhara kwa meli zilizotia nanga kwenye bandari".

Ilidai kuwa kiwanda cha Bajil kilifanya kazi kama "rasilimali kubwa ya kiuchumi", na kilitumiwa na kikundi hicho kujenga vichuguu na miundombinu, wakati maeneo ya bandari yalitumiwa "kwa uhamishaji wa silaha za Iran".

Bandari hiyo ni ya pili kwa ukubwa katika Bahari ya Shamu baada ya Aden, na ndiyo sehemu ya kuingilia kwa takribani 80% ya bidhaa za chakula zinazoagizwa Yemen.

Wakazi wengi waliliambia shirika la habari la Reuters kwamba zaidi ya mashambulizi 10 yalilenga Bandari ya Hudaydah na maeneo ya al-Salakhanah na al-Hawak jijini, huku mine mingine ikilenga kiwanda cha saruji.

Msemaji wa wizara ya afya inayoongozwa na Houthi, Anees al-Asbahi, alisema takribani watu 21 walijeruhiwa katika shambulio hilo.

Waasi wa Houthi walilaumu Marekani na Israel kwa pamoja kwa shambulio hilo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI