Mji wa Port Sudan - makao makuu ya serikali inayoongozwa na jeshi la Sudan na kitovu cha misaada ya kibinadamu kwa nchi hiyo - umekumbwa na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kwa siku ya tatu mfululizo.
Wanajeshi wa Sudan wanawalaumu waasi wa RSF, kwa kuhusika na mashambulizi hayo japo kundi hilo halijakiri kuhusika.
Maelfu ya watu wameuawa katika miaka miwili ya vita vikali kati ya jeshi na RSF na zaidi ya milioni 12 wamekimbia makazi yao.
Mashahuda wanaripoti kuona moshi mkubwa mweusi ukifuka kutoka maeneo tofauti jijini humo ikiwa ni pamoja na eneo linalozunguka bandari kuu na uwanja wa ndege.
Mashambulizi hayo yametatiza usafari katika eneo hilo.
Ndege hizo zisizo na rubani zinaripotiwa kulenga kituo cha umeme na hoteli.
Hadi siku tatu zilizopita, mji wa Port Sudan ulikuwa kimbilio la maelfu ya Wasudan walitoroka makaazi yao.
Ghasia za hivi karibuni, zimevuruga hali ya utulivu waliopata katika mji huo kwani vita vimekuwa vikiaendelea kwa zaidi ya miaka miwili.
Mashambulizi hayo ya ndege zisizo na rubani hapo awali yalilenga ghala la mafuta na kambi ya kijeshi.
0 Comments