Header Ads Widget

WAZIRI MKUU WA ISRAELI AKATAA UKOSOAJI WA VITA VYA GAZA NA WANAJESHI WA AKIBA


Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amekataa ukosoaji wa vita vya Gaza na baadhi ya wanajeshi wa akiba wa jeshi la anga, na kutaja tukio hilo kuwa "lisiloweza kusameheka".

Jeshi la Israeli lilisema kuwa litawafuta kazi wanajeshi wa akiba waliokuwa wametia saini barua ya kutaka kurejeshwa kwa mateka wa Israeli kupewa kipaumbele badala ya kupigana na Hamas.

Barua hiyo pia inasema mapigano ya sasa yamechochewa kisiasa na yatasababisha vifo vya mateka, wanajeshi wa Israeli na raia wasio na hatia.

Jeshi lilisema haliwezi kuruhusu wanajeshi wa akiba wanaohudumu kushiriki maandamano ya kisiasa.

Israeli ilianza tena kampeni yake ya angani na ardhini huko Gaza mwezi uliopita, ikisema kwamba shinikizo la kijeshi litailazimisha Hamas kuwaachilia mateka ambao bado inawashikilia.

Jeshi la anga la Israeli, ambalo limetumika sana huko Gaza katika kipindi cha miezi 18 iliyopita, linategemea sana marubani wa jeshi la akiba.

Idadi kubwa ya waliotia saini barua hiyo ambao ni 970 iliyochapishwa katika magazeti ya Israeli Alhamisi asubuhi wamestaafu. Lakini inaripotiwa kuwa kadhaa bado ni wafanyikazi.

Barua hiyo haitoi wito wa kukataa kuhudumu, lakini inadai "kurejeshwa kwa mateka wote hata kama itamaanisha ni kwa gharama ya kusitisha uhasama".

Jeshi la Israeli lilianzisha kampeni ya kuiangamiza Hamas kujibu shambulizi la kuvuka mpaka ambalo halijawahi kutokea tarehe 7 Oktoba 2023, ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 251 walichukuliwa mateka.

Zaidi ya watu 50,880 wameuawa huko Gaza tangu wakati huo, kulingana na wizara ya afya ya eneo hilo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI