Header Ads Widget

ZIMBABWE YAFANYA MALIPO YA KWANZA YA FIDIA KWA WAKULIMA WAZUNGU JUU YA KUNYAKUA ARDHI

 


Serikali ya Zimbabwe imetangaza malipo ya awali ya $3m (£2.3m) kwa wakulima wazungu ambao mashamba yao yalitwaliwa chini ya mpango wa serikali wenye utata zaidi ya miongo miwili iliyopita.

Ni malipo ya kwanza kufanywa chini ya makubaliano ya fidia ya mwaka 2020 yaliyotiwa saini kati ya serikali na wakulima wazungu wa ndani ambapo Zimbabwe ilijitolea kulipa $3.5bn (£2.6bn) kwa mashamba yaliyonyakuliwa.

Maelfu ya wakulima wazungu walilazimishwa kutoka katika ardhi yao, mara nyingi kwa jeuri, kati ya mwaka 2000 na 2001.

Unyakuzi huo ulikusudiwa kurekebisha unyakuzi wa ardhi enzi za ukoloni lakini ulichangia kuzorota kwa uchumi wa nchi hiyo na kuharibu uhusiano na nchi za Magharibi.

Malipo hayo yaliyotangazwa Jumatano ni ya wakulima 378 wa kwanza, kati ya 740 waliokuwa wamiliki wa mashamba ambao fidia yao ilikuwa imeidhinishwa.

Mnamo mwaka 1980, Zimbabwe ilipata uhuru, na kumaliza miongo kadhaa ya utawala wa wazungu wachache. Wakati huo, sehemu kubwa ya ardhi yenye rutuba zaidi ilikuwa ikimilikiwa na wakulima wazungu takriban 4,000.

Mageuzi ya aŕdhi yalilenga katika kugawa upya aŕdhi inayomilikiwa na wazungu kwa wakulima weusi, kufuatia seŕa za enzi za ukoloni wakati maelfu ya wakulima weusi walilazimishwa kutoka katika aŕdhi yao na maeneo yenye rutuba zaidi nchini humo yalitengwa kwa ajili ya watu weupe.

Mnamo mwaka wa 2000, Rais wa wakati huo Robert Mugabe aliunga mkono uvamizi wa ardhi uliofanywa na mseto wa vikosi vya serikali na vikundi vya kujihami, na hivyo kuzua shutuma za kimataifa.

Rais Emmerson Mnangagwa, ambaye alichukua nafasi ya Mugabe katika mapinduzi ya mwaka 2017, ametaka kutatua mzozo huo ili kurejesha uhusiano na serikali za Magharibi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI