Header Ads Widget

JE, DUNIA INAELEKEA KWENYE MDORORO WA KIUCHUMI?

 



Ushuru wa Rais wa Marekani Donald Trump umewasha moto katika masoko ya hisa ya kimataifa. Je, hilo linamaanisha tunaelekea kwenye mdororo wa kiuchumi?

Jambo la kwanza la kusisitiza ni kwamba kinachotokea katika soko la hisa - sio lazima wakati wote kiathiri uchumi - kushuka kwa thamani ya hisa haimaanishi kutatokea matatizo ya kiuchumi mbeleni. Lakini wakati mwingine hilo linaweza kuathiri.

Kuporomoka kwa thamani katika soko la hisa, kunamaanisha kuwa kuna tathmini ya msingi ya faida za siku zijazo kwa kampuni yanayounda soko la hisa la ulimwengu.

Kwa kiasi kikubwa, kile kinachotarajiwa katika masoko; ni kwamba ongezeko la ushuru litamaanisha gharama zitapanda na faida zitashuka.

Hilo halimaanishi mdororo wa uchumi utatokea, lakini nafasi ya mdororo kutokea ni kubwa zaidi kuliko ilivyokuwa kabla ya Trump kutangaza ushuru mpya na mpana.

Uchumi huelezwa kuwa uko katika mdororo, pale jumla ya vitu ambavyo sisi na serikali tunatumia au kuuza nje vitapungua kwa vipindi viwili mfululizo vya miezi mitatu.

Kati ya Oktoba na Desemba mwaka jana, uchumi wa Uingereza ulikua kwa 0.1%, na ripoti ya hivi karibuni ya kila mwezi inaonyesha umepungua kwa kiwango sawa na hicho mwezi Januari.

Makadirio ya kwanza ya jinsi uchumi wa Uingereza ulivyokuwa mwezi Februari, yatatolewa Ijumaa ijayo. Kwa hivyo, bado tuko mbali sana kuweza kusema tumefika katika mdororo.

Hata hivyo, katika ajali ya kuanguka kwa soko la hisa, kuna baadhi ya majeruhi wa kutisha na wanaotia wasiwasi.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI