NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani, Daniel Sillo, Apongeza Kampuni ya Asas chini ya mkurugenzi wake Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) Salim Abri Asas kwa Kudhamini Maadhimisho ya wiki ya Mabalozi wa Usalama barabarani kwa Miaka 6 sasa pamoja na kutoa Bima ya Afya kwa Familia 50 Iringa .
Waziri Sillo, alisema elimu ya usalama barabarani ndiyo Nyenzo muhimu katika kutokomeza matukio ya ajali kwani kwa aslimia kubwa zimeonekana zinatokana kuwa ni za makosa ya kibinadamu.
Aidha ameelezea kauli mbiu ya mwaka huu inayo sema "ushirikishwaji wa wanawake katika kuimarisha usalama barabarani ni nyenzo muhimu katika kuokoa maisha" na kuongeza kuwa kauli hiyo inatoa changamoto ya kupanua wigo wa elimu zaidi kutokana na waathirika wengi wa ajali hizo kuwa wanawake na watoto.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Kheri James, ambaye amemuwakilisha mkuu wa mkoa huo, Peter Serukamba, alishukuru shughuli hiyo kufanyika katika mkoa huo, pamoja na kuahidi kuendeleza ushirikiano pamoja na jeshi la polisi ili kuendelea kudhibiti ajali za barabarani.
Kwa upande wake mwakilishi wa kamanda wa usalama barabarani Ramadhani Ng'anzi Kamishana msaidizi wa polisi na CEO wa elimu na mafunzo ya usalama barabarani kwa umma, Michael Deleli, alisema jeshi hilo limeendelea kutoa elimu kwa jamii kwa kupanua wigo wa kuweka polisi kata kila eneo ili kuhakikisha elimu hiyo inamfikia kila mtu.
Kamanda Deleli alisema makosa ya usalam barabarani yamegawanyika katika makundi matatu ikiwemo, Makosa ya kibinadamu ambayo kwa asilimia 75 yanachangia ajali zote za barabaarani, Ubovu wa vyombo vya moto asilimia 25 pamoja na ubovu wa miundombinu, hivyo elimu inahitajika zaidi ili kutokomeza makosa hayo.
Awali akisoma risala ya taasisi yao, Mkurugenzi mtendaji wa bodi ya mabalozi wa usalama barabarni (RSA) Tanzania, Augustus Fungo, alisema wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii juu ya usalama barabarani kwa zaidi ya miaka 10 (10), kuripoti matukio ya ajali na ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani pamoja na kushawishi serikali juu mabadiliko ya sheria na sera za usalama barabarani.
Fungo, aliomba serikali kuangali upya sheria za usalama barabarani na kuzibadilisha kwani zimepitwa na wakati na kupelekea makosa ya barabarani kuendelea kuongeza kutokana na baadhi ya madereva kutokuwa na wasiwasi na sheria hizo.
"Eneo lingine linalotukwamisha ni eneo la mabadiliko la sheria za usalama barabarani, Mheshimiwa Mgeni rasmi, sheria hizi ni za zamani sana, na katika kila RSA day tumekuwa tukijaribu sana kukumbishia mara kwa mara, kwamba tunahitaji kubadili sheria za barabarabi kwa sababu ni za zamani na zina faini mpaka ya shilingi 1000" alisema Fungo.
Mnec Abri, alitaka kila mmoja kuwa balozi wa mwenzake katika kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua na hatimae kuisha kabisa.
"Nataka nijalilize katika shukrani, tumeshukuriwa kwamba miongoni mwa wadhani wanaodhamini shughuli za hawa ndugu zetu mabalozi na hasa elimu ya usalama barabarani, mimi kwa mtazamo wangu, na wengi mtakubaliana nami, hawa mabalozi endapo watu wangejua thamani ya hawa mabalozi na fikiri kila taasisi, kila NGO's ndani ya taasisi wanatakiwa wawe mabalozi au wananchama, tumepata kushuhudia ndani ya nchi yetu historia tumewahi kupoteza waziri mkuu ajali ya barabaraniTanzani, tumewahi kupoteza manaibu waziri, tumewahi kupoteza naibu Waziri Salome Mbatia mimi nakumbuka hapa Iringa alifia Njombe huko, tumepoteza maprofesa, tumepoteza madaktari, tumepoteza wanataaluma mbalimbali kwa hizi ajali barabarani, tumepoteza mpaka maiti, unasikia maiti inasafirishwa sehemu moja kwenda mfano inatoka Mbeya labda inapelekwa mkoa flani waliokuwepo kwenye gari wamekugfa na maiti imekufa tena"
"Kufa ni kufa kwa bahati mbaya tumekuwa tukiweka viwango vya kufa, hivi sisi tukienda kule kwenye makaburi yamewekwa kwa viwango yaani, huyu amekufa kwa ajali huyu amekufa ukimwi huyu amekufa kwa maradhi, kufa ni kufa kwanini akifa mwanasiasa mmoja nchi nzima inatikisika lakini wanaokufa kwa ajali tunanyamaza, kwanini, tuwapiganie hata wale wanaokufa kwa ajali hizi za barabaarani, nawapongeza sana RSA, ninyi ni watu wa maana sana ndani ya nchi hii, gari limebeba mgonjwa , linakwenda kuchukua mgonjwa linapata ajali mgonjwa na dereva wanakufa wote"
"Nani ambaye hatumii vyombo vya moto ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, hayupo hivyo ji jukumu letu kuhakikisha tuakwenda kuachana na ajali hizi, nawapongeza sana RSA mmekuwa mabalozi wazuri " alisema Asasi
Wanufaika wa bima hizo za Afya kutoka kampuni ya Asas Wamepongeza kampuni hiyo kwa msaada huo.
CHINI MATUKIO KATIKA PICHA MAADHIMISHO YA MIAKA 10 YA MABALOZI WA USALAMA BARABARANI KITAIFA MKOANI IRINGA.
0 Comments