Header Ads Widget

TAMKO LA KAMSHNA LAWAIBUA ACT WAZALENDO NA KUMUOMBA RAIS SAMIA AHARAKISHE UTEKELEZAJI WA RIPOTI YA HAKI JINAI


NA THABIT MADAI- ZANZIBAR matukiodaima3@gmail.com

CHAMA cha Act Wazalendo kimemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia suluhu Hassan kuharakisha utekelezaji wa ripoti ya haki jinai  ili  Jeshi la Polisi  liweze kufanya kazi kwa misingi ya haki na Uweledi.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa chama cha ACT  Wazalendo Othman Masoud Othaman kufuatia Tamko lililotolewa  hivi karibuni na Kamshna wa Jeshi la Polisi Zanzibar    CP. Hamad Khamis Hamad la kuwataka viongozi wa siasa kuacha kutumka vibaya uhuru kwa kutoa kauli matusi na kebehi kwa viongozi  wa Serikali na vyama vya siasa.

Amesema hatua hiyo ya Rais Dkt. Samia itasaidia kufikia lengo lake la kulifanyia mageuzi Jeshi la Polisi na kufanya kazi kwa uwadilifu na haki.

"Tunamuomba Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuongeza msukumo na kuharakisha utekelezaji wa ripoti ya Tume ya Haki jinai nchini ili kufikia lengo lake alilolitaja hadharani na kuwahidi watanzania kwamba jeshi la Polisi litafanyiwa mageuzi makubwa," amesema.

"Miongoni mwa kasoro kubwa za kimfumo wa Utekelezaji  wa haki za polisi unaohitaji mageuzi ya haraka ni ule hasa ngazi za mikoa kuchukua amrita za kisiasa kwa masuala ya haki za watu kutoka kwa wakuu wa mikoa na wilaya ambao baadhi yao so waadilifu,wanakiuka katiba na sheria za nchi katika utendaji wao,"  amesema.

Mwenyekiti huyo ambae ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar  amelitaka Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa misingi iliyoweka na kuacha kuegemea upande mmoja wa kisiasa.

"Jeshi la Polisi bado wanayo nafasi ya kufanya kazi zao kwa uadilifu, hivyo liache kujiegemeza upande mmoja wa siasa, amesema

Hata hivyo ameeleza kuwa chama hicho kitasamia maoni ya Wanachi ya kutoshirikia uchaguzi Mkuu kwa siku mbili.

Mkutano na Waandishi wa Habari umefanyika katika ofisi ndogo za chama hicho Vuga Mjini Magharibi Unguja.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI