Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na mmiliki wa AYO TV na millardayo.com, Bw. Millard Ayo (kulia) alipowasili kwenye viwanja vya maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Jumuiya ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA) kuhusu Miaka Mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Uhuru wa Vyombo vya Habari . Kongamano hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa Maktaba ya UDSM mkoani Dar es salaam, Mei 21, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Jumuiya ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA) kuhusu Miaka Mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Uhuru wa Vyombo vya Habari wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipozungumza katika Kongamano hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam mkoani Dar es salaam, Mei 21, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Kongamano la Jumuiya ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA) kuhusu Miaka Mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Kongamano hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) mkoani Da es salaam, Mei 21, 2024.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mtandao wa Kijamii Fullshangwe, John Bukuku akiwasilisha Mada katika Kongamano la Jumuiya ya Wanahabari wa Mitandao ya Kijamii iliyofanyika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa.Kogamano hilo limefanyika leo Mei 21,2024 Jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi wa Matukio Daima media Francis Godwin katikati akiwa na Wanahabari wa mitandao kutoka mkoa wa Mwanza na Kagera
Mkurugenzi wa Matukio Daima media Francis Godwin kushoto akiwa na washiriki wa kongamano la JUMIKITA
Mwanahabari Zacharia Nyamoga toka Iringa akiwa kwenye Banda la Global
0 Comments