Header Ads Widget

MAKONDA AKERWA NA MIVUTANO YA MADIWANI, MBUNGE NA HALMASHAURI YA JIJI ARUSHA

  

   MKUU WA MKOA WA ARUSHA PAUL MAKONDA


 MATUKIO DAIMA APP, ARUSHA.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amekemea tabia ya malumbano na kuvutana kwa watumishi na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha kwani jambo hilo  limesababisha kukwama kwa miradi mingi ya maendeleo licha ya Serikali kutoa fedha nyingi za kutekeleza miradi hiyo.

 

Ametoa kauli hiyo leo, mara baada ya kupokea ripoti ya utendaji wa Wilaya ya Arusha, iliyoonyesha kukwama kwa miradi mingi ya maendeleo kutokana na mabishano, malumbano na kutokuelewana kati ya Menejimenti ya Wilaya, Baraza la madiwani na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini.


Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtahengerwa, amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa migongano hiyo ya kutokuelewana kati ya viongozi wa kuteuliwa na kuchaguliwa kumesababisha adhabu kubwa kwa wananchi kutokana na miradi muhimu kukwama na hivyo kuwachelewesha kimaendeleo.

 

"Ingekuwa ni mamlaka yangu ningevunja Mamlaka yote ya Jiji la Arusha maana siobi umuhimu wa Jiji kuwepo katika kuwaletea maendeleo wananchi" alisema Makonda.

 

Kufuatia hali hiyo, Makonda, amelitaka Baraza la Madiwani Jiji la Arusha kujitafakari na kuamua kuwa sauti ya wananchi kikamilifu na kupambana kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana kwa kukamilisha miradi yote ya maendeleo kwa wakati.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI