Header Ads Widget

MBUNGE KABATI AKABIDHI VITANDA ZAHATI YA BOMA LA NG'OMBE

 

Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa Mh Ritta Kabati ametoa msaada wa vitanda 4, magodoro 4 na mablangeti katika zahanati ya kata ya Boma la Ng'ombe iliyopo wilaya ya Kilolo.


Kabati ametoa nsaada huo wakati wa hitimisho la wiki ya vijana wilaya ya Kilolo iliyofanyika katika kata ya Boma la Ng'ombe.


Kabati amesema msaada huo wa vitanda na magodoro utapunguza changamoto ya kukosekana kwa vitanda kwa wagonjwa wanaotakiwa kupumzishwa kabla ya kupata rufaa.


Katika hatua nyingine Kabati ametoa msaada wa sukari, sabuni na chumvi kwa wazee wiojitokeza katika hadhara ya kukabidhi vitanda hivyo.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI