Header Ads Widget

SIMBA JESSE ASHAMBULIWA HADI KUFA NA WAPINZANI WAKE

Matukio Daima App, Kenya.

Wakenya wanaomboleza kifo cha simba wa kuhamahama, Jesse, aliyefariki baada ya mapigano ya kimaeneo na mpinzani wake huko Maasai Mara.


"Alikuwa simba mzuri," lilisema shirika la Mara Predator Conservation Programme (MCPC) katika kutoa heshima zake kwenye Facebook.


Taarifa za kusikitisha za simba aliyejeruhiwa vibaya awali zilitolewa na Shirika la Hifadhi ya Mara Kaskazini (MNC).


Licha ya usaidizi wa haraka, Jesse ambaye alikuwa na umri wa miaka 12, hakuweza kunusurika katika shambulio hilo na alikufa kutokana na majeraha yake. Alizaliwa ndani ya MNC mapema 2011, Jesse na kaka yake Frank. Mnamo 2014, ndugu hao waliachana na kuchukua uongozi katika kundi jingine la simba.

Wakati wao kama viongozi, Jesse na Frank walikuwa na watoto kadhaa. Ingawa wana wao wamekufa au wamepotea, binti zao wanasemekana "kuendeleza jamii yao."


Mnamo mwaka wa 2016, Frank alipotea na Jesse akaanza maisha ya kuhamahama na ya kujitenga zaidi ingawa bado alikuwa akionekana katika hifadhi mbalimbali mara kwa mara.


Jesse alirejea MNC mapema 2023, hata hivyo eneo ambalo aliwahi kutawala na kaka yake lilikuwa na viongozi wapya - wanaume wa Engoyanai. Ugomvi mbaya na wao ulisababisha kifo chake cha ghafla mnamo 24 Julai.


Muda wa wastani wa maisha wa simba ni takriban miaka 13 porini, ingawa wanaweza kuishi muda mrefu zaidi wakiwa wanatunzwa mahali pamoja.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI