Header Ads Widget

WAFANYABIASHARA MKOANI TANGA WAPIGWA MARUFUKU KUFANYA BIASHARA MAENEO YA BARABARANI

  



NA AMINA SAIDI,TANGA



Halmashauri ya jiji la Tanga imewaelekeza wafanyabiashara wa jiji la Tanga wanaofanya biashara katika maeneo ya  barabara zisizofungwa kwa matumizi hayo waache mara moja na kuhakikisha zinakuwa salama kwa matumizi ya vyombo vya moto.


Hayo aliyasema mstahiki Meya wa jiji la Tanga  Abdarahman Shillow katika baraza la madiwani  la Halmashauri ya jiji Tanga  ambapo aliwaomba mkurugenzi wa jiji  pamoja na uongozi wake wote kulisimia suala hilo.


Aidha alisema kuwa wafanyabiashara kufanya biashara nje ya maduka yao  na kuweka barabarani ni kuhatarisha maisha ya watumiaji wa barabara hizo  pamoja na watumiaji wa vyombo vya moto.


Aliwaomba watendaji wote wa halmashauri kwa kushirikiana  na Mkurugenzi wajiji Bi.Sipora Liana  kuweza kulisimamia hilo kwa yoyote  atakaekiuka maelekezo hayo achukiliwe hatua za kisheria.


Sambamba na hayo katika baraza hilo  mstahiki meya wa Jiji  la Tanga pamoja  na mkurugenzi walimpongeza Diwani wa kata ya Mnyanjani kayaga simba ambaye alichukukua nafasi aliyekuwa Diwani kutangulia mbele ya haki.


Mh.Simba alipita kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika mwishoni mwa mwezi wa kumi na mbili mwaka uliopita kupitia tiketi  chama cha mapinduzi CCM  mkoa Tanga. 


Aidha katika baraza  hilo pia mh.Kayaga Simba  aliapishwa kwenye baraza hilo   na kushiriki baraza la madiwani akiwa kama diwani wa kata ya mianjani  kupitia Chama tawala CCM. 


Akizungumza mara baada ya baraza hilo  Diwani Simba alisema yupo tayari kushirikiana wananchi wa kata ya mianjani katika kuhakikisha  kero zao zote zinapatiwa majibu  kama ilivyo ilani ya chama chama mapinduzi.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI