Akitangaza matokeo hayo jana msimamizi mkuu wa
uchaguzi huo kanali Laban
Thomasi alisema kuwa kwa
upande wa uenyekiti
wagombea walikuwa watatu
ambapo Daud Yassin alishinda kwa kupata kura 481
kati ya kura 651
zilizopigwa huku Dkt Neema Chaula
akifuatia kwa kupata kura 122 na Anna Mlalambia akipata kura 48.
Katika nafasi ya Halmashauri kuu ya
CCM Taifa (NEC) akiwakilisha
mkoa wa Iringa wagombea walikuwa watatu ambao aliyekuwa MNEC
kipindi kilichopita Salim Abri
Asas akifanikiwa kutetea nafasi
yake kwa
kupata kura 593
sawa na asilimia 92 ya
kura halali 645 huku akiwashinda
wapinzani wake Mgambe Kihongosi
aliyepata kura 34 na Dkt. Alex
Elia Sanga akipata kura 18.
Kwa
upande wa nafasi ya mjumbe wa
halmashauri kuu CCM mkoa ambapo kuna nafasi mbili kila wilaya kwa Wilaya ya
Kilolo ni Seki B. Kasuga alishinda kwa kupata kura 513 huku wa
pili akiwa ni Leah V. Mwamoto
aliyepata kura 340
Wilaya ya Mufindi ni Dickson H. Mwipopo aliyepata kura 480 na Godfrey Mosha aliyepata kura 246, Wilaya ya Iringa Vijijini ni Christopher S. Mahembe aliyepata kura 309 na Kanuth T. Mhongole aliyepata kura 212 na Wilaya ya Iringa Mjini ni Tumaini G. Msowoya aliyepata kura 488 na Vitus S. Mushi aliyepata kura 297.
0 Comments