Header Ads Widget

KOCHA SIMBA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA


 

Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) inawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya miongoni mwao akiwa ni Kocha wa Makipa wa Simba sc Muharami Mohamed maarufu kama ‘Shilton’.

 

Hayo yameelezwa leo Novemba 15, 2022 na Kamishna Jenerali wa DCEA, Gerald Kusaya alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

 

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mamlaka hiyo imesema iliendesha Operesheni katika maeneo mbali mbali nchini na kukamata Jumla ya Kilo 34.89 za dawa za kulevya aina heroin pamoja na kukamata biscuit 50 zilizotengenezwa kwa kutumia dawa za kulevya aina ya Bangi kama moja ya Malighafi.

 

Mtuhumiwa mwingine miongoni mwa hao waliokamatwa ni Kambi Zubeir Seif ambaye ni Mfanyabishara na Mmiliki wa Kituo cha Michezo cha Cambiasso kilichopo Tuangoma, Kigamboni Dar es Salaam na pia ni mmiliki wa Kampuni ya Safia Group of Companies ambayo ina miliki magari ya kusafirisha abiria (daladala) kutoka jijini Dar es salaam Kwenda mkoa wa Pwani, na Said Matwiko mkazi Magole jijini Dar es salaam.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI