Header Ads Widget

SIMBA YAMKATAA KOCHA ALIYEKAMATWA KWA TUHUMA ZA MADAWA YA KULEVYA.

 


Muda mfupi baada ya kutolewa kwa taarifa ya Kocha wa Makipa wa Klabu ya Simba, Muharami Said Sultan kukamatwa kwa tuhuma za kukutwa na madawa ya kulevya aina ya Heroine, Klabu hiyo imetoa tamko na kueleza kuwa hakuwa mwajiriwa wa klabu hiyo.


Taarifa iliyotolewa na Menejimenti ya Klabu ya Simba, imeeleza kuwa Muharami hakuwa mwajiriwa bali aliombwa kuwanoa makipa kwa muda wa mwezi mmoja wakati klabu ikiendelea kutafuta kocha wa magolikipa.

 

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, haihusiki na tuhuma zinazomkabili kocha huyo na kuwataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa watulivu kwani hakuna athari yoyote inayoweza kuikumba klabu hiyo kutokana na kadhia iliyomkumba kocha huyo.

  

Taarifa ya Muharami pamoja na watuhumiwa wengine 8 kukamatwa, zimetolewa leo na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Gerald Kusaya wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI