Header Ads Widget

MRADI WA YAM NA HALMASHAURI YA MUFINDI WATOA MAFUNZO YA KUTENGENEZA PIKIPIKI KWA VIJANA MAZINGIRA MAGUMU

MRADI wa Youth Agency Mufindi (YAM) na 

Halmashauri ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa waanza kutoa mafunzo ya kutengeneza  pikipiki Kwa vijana 48 kutoka kwenye mazingira magumu ili kupunguza ukali wa Maisha .

Wakizungumza jana wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea Ukumbi wa Yatima Igoda Mufindi washiriki wa mafunzo hayo Anold Kalinga na Zedani Kabonge  mbali ya kupongeza mradi wa YAM Kwa mafunzo hayo Bado wamesema mafunzo hayo ni mwanzo wa kuondokana na tatizo la ajira kwao .

Walisema kabla ya kuunganishwa na mradi huo wa YAM walikuwa wakilazimika kushinda vijiweni na baadhi yao kushawishika kujiingiza Katika makundi hatarishi ya ulevi na mambo yasiyofaa.

Hivyo walisema kupitia mradi wa YAM na mafunzo wanayopatiwa ni wazi watakwenda kuwa tofauti na vijana wenzao na kuanzisha vijiwe vya kazi ya ufundi pikipiki vijijini kwao .
 
Huku mkufunzi wa mafunzo hayo Said Hassan akieleza mafanikio ya mafunzo hayo toka alipoanza kuwa vijana wameanza kuonesha mwanga wa kuwa mafundi .



Mradi huo unatekelezwa na Halmashauri ya Mufindi chini ya mradi wa Foxes  Community and Wildlife Conservation( FCWC) na YAM kupitia ufadhili wa Finland utakelekelezwa kwenye kata za Luhunga ,Ihanu na Mdabulo ni mradi utanufaisha  vijana na  watoto  wanaotoka  katika  familia duni zaidi ya   vijana 770  atika  vijiji 16.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI