Header Ads Widget

KAMATI YA BUNGE HUDUMA ZA JAMII YATAKA CHUO CHA RUNGEMBA KIPEWE BAJETI ZAIDI

 


WAJUMBE   wa kamati ya  kudumu ya bunge ya  huduma  na  maendeleo ya  jamii wameshauri  serikali   kuongeza bajeti  kwa  chuo  cha maendeleo ya jamii Rungemba  wilayani  Mufindi  mkoa wa Iringa  ili  kusaidia  kufanya  maboresho makubwa ya majengo ya  chuo  hicho ambayo ni  chakavu.


wakizungumza    wakati  wa ziara   ya kukagua maendeleo ya  chuo  hicho   wajumbe hao  ambao waliambatana na naibu  waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii, Mwanaidi Ali Khamis pamoja na katibu  wa  wizara  hiyo, kuwa  pamoja  na  serikali  kutoa kiasi cha  shilingi  milioni 500 kwa  ajili ya  ukarabati wa  chuo  hicho  ila bado  fedha  hizo  ni  ndogo  sana  kulingana na hali  halisi ya  uchakavu  wa  miundo  mbinu ya  chuo hicho .

wajumbe  Aloyce  Kamanda   na  Paulina  Nahato   walisema  kuwa  pamoja na  jitihada  kubwa  zinazofanywa na serikali  chini ya  Rais  Samia Suluhu Hassan  kutoa  fedha  za  uboreshaji  wa  miundo  mbinu ya   vyuo  vya maendeleo ya  jamii  nchini ila  bado kwa  hali  ilivyo  chuo  cha Rungemba  kinahitaji  fedha  zaidi  kwa  ajili ya  ujenzi  wa majengo mapya na  sio ukarabati  kutokana na majengo  yaliyopo  kuzeeka .


Hivyo  walishauri  uongozi  wa  chuo  hicho  pamoja na  wizara  husika  kukaa pamoja na kufanya  tathimini ya  kina ili  kuandaa bajeti  kubwa zaidi  itakayopelekwa  bungeni  ili  wao kama  wajumbe  wa kamati  husika  waweze  kuipigania bungeni  ili  bajeti  hiyo  ipite kwa  ajili ya uboreshaji mkubwa wa  chuo  hicho.

Mbunge Nahato  alisema  chuo  hicho  mama  yake mzazi  amepata  kusoma   hapo  na hali ya  majengo  iliyokuwepo  wakati  huo kwa  sasa ni mbaya  zaidi  hivyo  kuona  majengo  hayo yanakarabatiwa  kwa  upande  wake  anaona  si sawa  kwani  ilipaswa majengo kujengwa mapya kabisa .

Mwenyekiti  wa kamati  hiyo Stanslaus Nyongo  alisema  kuwa  kamati  yake  imeridhishwa na kasi ya  maendeleo katika  chuo   hicho .


Pamoja na  kuona   hali ya  chuo  hicho  ikiwa mbaya zaidi  kutokana na  uchakavu  wa  miundo  mbinu   mbali ya  jitihada  kubwa  ambazo serikali  imeendelea  kufanya .

Hivyo  alisema   mategemeo ya  kamati  hiyo  kuona  serikali  inakwenda  kutekeleza  ushauri  mbali mbali  ambao  umetolewa na  wajumbe wa kamati  hiyo  ili  kuwezesha  mazingira ya  vyuo  hivyo  kuwa  bora  zaidi .


Alisema kuwa, ukarabati na ujenzi wa miundombinu chuoni hapo yakiwemo mabweni na jengo la Utawala ni suala la lazima kwani itasaidia kuweka mazingira mazuri ya wananfunzi kufundisha na kujifunzia kwa kupata sehemu nzuri ya kulala na kushiriki masomo vizuri.

 

Aidha  Nyongo alielekeza Wizara kuainisha maeneo yanayojitaji mchango wa Wabunge ili yatafutiwe ufumbuzi wa haraka ikiwemo kupatiwa fedha za maendeleo ili waweze kuboresha miundombinu Chuoni hapo.

 

"Pamoja na ripoti hii, nampongeza Mkuu wa Chuo ametueleza hali ya chuo na miradi inayotekelezwa lakini hali ni mbaya hatuwezi kufumba macho." alisema Nyongo.  

 

Akizungumza mbele ya Kamati hiyo Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Ali Khamis alisema Wizara itatekeleza maelekezo ya Kamati na zaidi itahakikisha malengo ya kuboresha elimu yanafikiwa.

 

Naibu Waziri Mwanaidi alisema, Kamati hiyo ina mchango mkubwa katika kusukuma mbele mipango ya Wizara ikiwemo uboreshaji wa miundombinu vyuo vya maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii.

 

Katibu Mkuu wa Wizara Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula amesema Juhudi za kuboresha mazingira ya Vyuo vinavyosimamiwa na Wizara zimeanza.

 

"Waheshimiwa Wabunge kama mnavyoelewa, hii ni Wizara mpya ambayo timekabidhiwa tarehe 10 Januari, nasi tumeanza kutafuta mbinu za kutafuta ufumbuzi matatizo mbalimbali. Lakini tunashukuru kwamba mmejionea hali ilivyo tutaendelea kutembea pamoja kuleta mabadiliko" alisema. 

 

Awali akiwasilisha taarifa, Mkuu wa Chuo cha Rungemba, Kidubya Kulamiwa alisema Chuo kimeanza kufanya ukarabati wa miundombinu ya ikiwemo jengo la Utawala na Jengo la uokaji.

 

Kulamiwa alisema sambamba na hatua za ukarabati, Chuo kinaendesha miradi ya kilimo cha ufugaji wa nyuki, parachichi, ufugaji wa Samaki na mradi wa Uokaji mikate na kusindika bidhaa zinazotokana na mazao ili kuboresha lishe hasa kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa. 




























Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI