Header Ads Widget

MNEC ASAS ACHANGIA MILIONI 5 UVCCM TAWI LA CHUO KIKUU CHA IRINGA

Mjumbe  wa Halmashauri kuu ya  CCM Taifa (NEC)  Salim Abri  Asas (kulia)  akimkabidhi jana mwenyekiti wa UVCCM tawi la  chuo kikuu  cha Iringa Daud  Lukanguji  kiasi  cha shilingi milioni 5  ambazo  alichangia kupitia mnada wa keki iliyoandaliwa na  UVCCM tawi  hilo  kuchangia uboreshaji wa mfuko  wa  kusaidiana  chuoni Picha na Francis Godwin

MJUMBE  wa  Halmashauri  kuu  ya chama  cha mapinduzi Taifa (NEC)  Salim  Asas amechangia  kiasi cha shilingi milioni 5  kuwezesha   kukufuliwa  kwa  mfuko  wa  kusaidiana  wakati  wa  shida kwa  wanachama  wa   umoja  wa  vijana  wa chama cha mapinduzi (UVCCM) tawi la  chuo  kikuu cha Iringa .

Akizungumza  baada ya  kuchangia fedha  hizo jana kupitia  mnada wa  keki iliyoandaliwa na  wanachama hao  chuoni hapo  Asas alisema   kuwa  suala la wanachama  wa  tawi  hilo la  chuo  kikuu  cha  Iringa  kuwa na  mfuko  wao  wa  kusaidiana ni jambo la msingi  na  litasaidia  kupunguza  changamoto  za  wanachama  pindi  wanapokwama .

Kuwa  kupitia  mfuko   huo  wa  kusaidiana  utakaoanzishwa  ni hatua  moja  wapo  ya  wanachama   kuondokana na kero ya kutafuta njia ya  kumsaidia  mwanachama   mwenzao pindi anapopatwa na shida .

“ Pamoja na  kufikiria  kuanzisha  mradi  wa tawi  ila  hili la  kuanzisha  mfuko  wa  kusaidiana kwenu  ninyi  ni ukombozi  mkubwa maana  wakati  mwingine  unakuta  mwanafunzi  mwenzenu anakabiliwa na changamoto ya laki moja  ili  kutatua changamoto  yake  pindi anaposubiri mambo yake ya  kifedha  kuwa  vizuri  inakuwa  rahisi  kukopeshana  kupitia mfuko  huu” alisema

Pia  alitaka  suala la  kuanzisha  ujenzi  wa  ofisi ya UVCCM tawi la  chuo  kikuu cha Iringa  kufanyiwa kazi  haraka  ili  kuweza  kuwa na  ofisi  itakayofanya  shughuli  za  chama .

MNEC  Asas  alisaema   kwa  upande  wake  amekuwa  mdau  mkubwa  wa  chuo    hicho  cha Iringa pamoja na  kuhakikisha  wanachama  wanaendelea   kutimiza  majukumu yao ndani ya  tawi hilo .

Hata  hivyo  alisema   ili  tawi  hilo  kuweza  kufanikiwa  zaidi ni lazima  kuwa na malengo  sahihi ya  kukitumikia  chama  badala ya  kutaka  chama  kiwatumikie kwani  wapo  baadhi  ya  watu  wanajiunga na  chama  ili  kutafuta  nafasi  za  uongozi jambo  ambalo  si  sawa .

Kuwa nafasi  za  uteuzi ndani ya  chama na  serikali ni nafasi ambazo  zinakuja  zenyewe   na sio  kuzitafuta  kwa  nguvu  pale unapofanya vizuri kwenye chama  ndipo  mwanzo  wa  kuteuliwa na  sio wewe  kutafuta  teuzi .

Aidha  aliwataka   wanachama wa  CCM  kila  mmoja kwa nafasi yake  kuendelea  kueleza  mambo  mazuri na makubwa  ambayo Rais Samia  Suluhu  Hassan  amekuwa akiyafanya katika  taifa   hilo  kwa  kusimamia  miradi mbali mbali ya  maendeleo .

Awali wakizungumza  katika  hafla   hiyo  makada wa  CCM Itiwen  Samson na  Richard Kasesela   walisema  kuwa  mchango  wa MNEC  Asas  katika maendeleo  ya Iringa ni mkubwa  sana na  kuwa ni  vigumu  kuyaelezea .

Kasesela  alisema  kuwa pamoja na  Asas  kusaidia chama  ila  amekuwa  msaada  mkubwa  wa kuchangia  maendeleo ya  mkoa  wa Iringa katika afya ,elimu na hata mtu  mmoja  mmoja wakiwemo  wanafunzi  kuwasaidia  kusoma.

Mwenyekiti  wa UVCCM Tawi la   chuo  kikuu cha Iringa  Daud  Lukanguji akishukuru kwa mchango  huo  wa  shilingi  milioni 5  kwa  ajili ya  kuanzisha mfuko  wa kusaidiana  chuoni hapo  alisema  hatua  hiyo ni kubwa  sana kwao  kuanza mfuko  huo .

Alisema  kuwa mfuko   wa  tawi  ulikwisha  anzishwa  japo  haukuwa na fedha  yoyote na ndio  sababu ya  kuandaa keki  hiyo  ili  kuiuza kwa mnada na  fedha  ambayo  wangepata  ingesaidia   kuboresha  mfuko  huo  hata  kuanzisha  biashara yoyote itakayosaidia  kutunisha  mfuko  huo  hivyo kwa  kiasi  hicho alichotoa MNEC ni  kikubwa  zaidi  kuufanya mfuko  kufanya kazi  vizuri .




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI