Header Ads Widget

MWANAFUNZI WA MIAKA 13 SHULE YA MSINGI AHUKUMIWA KWENDA JELA

 


Picha ya mtandaoni haihusiani na habari hii

Mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Makete mkoa wa Njombe imemhukumu  mwanafunzi wa shule ya msingi Lupalilo (13) kwenda jela miezi sita na kulipa Faini 8500 kwa makosa ya wizi wa vitu mbalimbali, imetolewa

Huku Anna Sanga (36) wa kijiji cha Lupalilo wilayani  aliyeshitakiwa pamoja na mwanafunzi huyo akiachiwa huru .


Washtakiwa walifikishwa mahakamani hapo  Septemba 4, 2021 majira ya saa 5 asubuhi huku  mlalamikaji akiwa  Sara Sanga (50) ambae alidai kuibiwa  vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi laki 8 na elfu 85 ambavyo ni mali yake halali

Hata hivyo upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha ushahidi wake dhidi ya mshtakiwa wa kwanza ambaye ni Anna Sanga baada ya kukosekana kwa ushahidi wa kumtia hatiani pasipo shaka

Mahakama hiyo imemhukumu mwanafunzi huyo wa shule ya msingi Lupalilo kifungo cha nje cha miezi sita na kulipa faini ya shilingi 85,000 kwa mlalamikaji 

Hukumu hiyo imetolewa Novemba 5, 2021 na Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Makete Mh. Ivan Msaki pamoja na mwendesha mashtaka wa serikali Asifiwe Asajile.

Chanzo;Greenfm radio Makete

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI