Uzinduzi wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwl Julius Kambarage Nyerere unatarajiwa kufanyika Nov 6, 2021 katika ukumbi wa kimataifa wa Mwl.Julius Nyerere International Convetion Centre jijini Dar es salaam. mwandishi wa matukio daima Fatma Ally anaripoti kutokea Dar Es Salaam.
Katika taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa Taasisi hiyo, Moshi Said inaeleza kuwa, hatua hiyo imekuja mara baada ya kufanyika mkutano Mkuu wa wanachama wa Taasisi hiyo mbele ya Mwenyekiti wake Mh. Paul Kimiti wakati akizungumza na wanachama waliohudhuria mkutano huo uliofanyika Oct 24, 2021 katika ukumbi wa Msasani Beach kawe jijini Dar es salaam.
Kupitia kwa katibu Mkuu wa Taasisi hiyo Mh.Simon Rubugu baada ya kushauriana na Mwenyekiti na wajumbe bodi kwa pamoja amesema uzinduzi wa tukio hilo muhimu la kitaifa na la kihistoria litafanyika kama ilivyopangwa na halitoahirishwa.
Aidha katika hatua nyingine ndani ya Mkutano huo wa wanachama wa Taasisi hiyo kulifanyika harambee ya kusaidia kuwezesha Maandalizi ya uzinduzi, kwa wanachama mbalimbali kujitokeza na kujitolea kuchangia kwa hiari ili kufanikisha tukio hilo muhimu la uzinduzi.
Katika harambee hiyo jumla ya shilingi Laki tano na themanini na tano (5.85 ) zilipatikana zikiwa ni fedha taslimu ukumbini hapo huku shilingi milioni tano laki tatu na hamsini na tano elfu zikiwa ni ahadi(5.355) kutoka kwa baadhi ya wanachama hao waliohudhuria katika mkutano huo.
Pia katika mkutano huo wanachama mbalimbali waliokamilisha fedha za usajili wa uanachama walipata usajili wa kutambulika rasmi kwa mujibu wa katiba ndani ya taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kupatiwa kadi na Tshirt kwa waliokamilisha fedha za malipo kwa huduma hizo kabla ya tukio lenyewe la uzinduzi.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na wanachama kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini, Pia ulihudhuriwa na viongozi kadhaa waliohudumu serikalini kitaifa akiwemo Spika Mstaafu wa Zanzibar Mh.Pandu Ameir Kificho, Mh Prof.Anna Tibaijuka Mh.Zakhia Meghji, Mh.Dkt.Maua Daftari, Mh.Bi Imelda Mutafungwa pamoja na Mh.Wilson Mukama
Viongozi hao wastaafu kwa nyakati tofauti hawakusita kutoa pongezi zao za dhati kwa Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mh.Paul Petro Kimiti na sekretarieti yake kwa namna ilivyojipanga katika kuhakikisha Taasisi hiyo inayaenzi yale yote yaliyokuwa yakifanywa na hayati Baba wa Taifa Mwl.JK Nyerere enzi za uhai wake.
0 Comments