Na Hadija Omary _Lindi
Ikiwa leo ni oktoba 15 ambapo Mataifa yote ulimwenguni yakiadhimisha siku wanawake vijijini , Wanawake wa kata ya Mtama Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi wamemshukuru Rais Samia Suluhu kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya katika kata yao.
Wakizungumza na Matukio Daima Wanawake hao walisema kuwa ujenzi huo wa kituo hiko cha Afya utaenda kupanua huduma za uzazi pamoja na huduma zingine walizokuwa wakizipata kutoka katika zahanati pamoja na kupunguza gharama ya kusafiri kwenda Hospital ya Nyangao kwa ajili ya kupata huduma
Nae Melina kambona Mkazi wa Mtama alisema kuwa kwa sasa wananchi hao wanapata huduma katika ngazi ya zahanati ambapo kulingana na wingi wa wagonjwa wanaoenda kupata huduma katika zahanati hiyo ulazimika kuchukuwa muda mrefu kusubiri huduma na pengine kwenda hospitali ya nyangao kupata huduma zingine ambazo kwenye zahanati hiyo haipatikani
Alisema uchache wa vifaa na wahuduma ukilinganisha na wagonjwa wanaofika katika zahanati hiyo pia ni changamoto kwani wakati mwingine mpaka mama anaweza kujifungua nje kabla ya kuanza kupatiwa huduma
"Kwa mfano sasa hivi mjamzito uchungu ukimuanza anapelekwa zahanati unaweza ukakuta wajawazito wengine wako pale wanapata huduma na vile madaktari walivyokuwa kidogo kwa hivyo nuss anajitahidi kadili ya uwezo wake ili kumsaidia ila lakini utakuta mama yule anajifungulia pale pale nje kabla hajaingia ndani kutokana na uhaba wa vifaa" alifafanua
Nae Fatuma seleman alisema kuwa kituo hiko kitakapokamilika kitawawezesha kupata huduma za uzazi kwa urahisi hivyo anamshukuru Rais Samia kwa kutoa kiasi hiko cha fedha kwa ajili ya ujezi wa kituo cha Afya
" Tunamshukuru sana mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kutusogezea huduma hii karibu kwani sasa tutakwenda kupata huduma ya uhakika hata upasuaji wa uzazi tupata hapa" alisema fatuma
Nae Salum Chande alisema Kutokana na kokosa kwa baadhi ya huduma katika zahanati hizo akinamama walikuwa wakisafiri kwenda Hospital ya nyangao jambo ambalo ilikuwa usumbufu na pengine kupelekea mpaka kifo kwa mama mjamzito akiwa njiani kuelekea Hospital.
Kwa upande wake Abruhami juma Mhadisi wa ujenzi Halmashauri ya Mtama alisema fedha za Mradi huo zimetokana na makato ya miamala ya simu ambapo kwa awamu ya kwanza utahusisha Majengo ya mahabara, kichomea taka pamoja na jengo la wagonjwa wa nje na unatarajiwa kukamilika mapema mwezi Desemba mwaka huu.
Hata hivyo aliongeza kuwa mara baada ya Kukamilika kwa Mradi huo wa kituo cha Afya Wananchi wa Mtama wataweza kupata huduma za X_Rey, Jengo la Uzazi na Mahabara ambozo katika Zahanati waliyokuwa wanapata huduma hazikuwepo.
0 Comments