Header Ads Widget

WATU WALIOJIHAMI WATEKA MELI YA MIZIGO NA KUIELEKEZA SOMALIA

Shirika la usalama wa baharini la Uingereza limesema kuwa, meli moja ya mizigo iliyokuwa ikisafiri katika Ghuba ya Aden imetekwa na watu sita wenye silaha ambao wamielekeza kuelekea Somalia.

Tukio hilo limetokea wakati kuna ongezeko la mashambulizi ya maharamia wa Somalia baada ya zaidi ya muongo mmoja wa kupungua kwa visa hivyo.

Tukio hilo pia limetokea wakati Iran imekuwa ikitishia kwamba washirika wake, wanamgambo wa Kihouthi nchini Yemen, watazuia meli zinazopita katika Bahari Nyekundu kupitia Ghuba ya Aden.

Bado haijafahamika ni nani aliyeiteka meli hiyo, lakini tukio hilo, ni la hivi karibuni zaidi tangu kuongezeka tena kwa shughuli za uharamia wa Somalia tangu mwezi Aprili.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI