Header Ads Widget

VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUWA KIELELZO CHA UAMINIFU

 

Nassor Mnambila ,
Kamishna Ofisi ya Rais ya Utumishi wa Umma


Mameya,Wenyeviti wa Halmashauri nchini wakutanishwa kwenye mafunzo ya maadili


Na Lilian Kasenene,Morogoro, Matukio DaimaApp 


VIONGOZI wa umma wametakiwa kuwa kielelezo cha uaminifu, uwazi, usawa na uzingatiaji sheria katika maamuzi yao ya kila siku.

Kamishna wa maadili ofisi ya rais sekretarieti ya maadili ya viongozi, Jaji mstaafu Sivangilwa Mwangesi  amesema maadili yanasaidia kuzuia migongano ya maslahi, matumizi mabaya ya madaraka, rushwa na upendeleo.

"Maadili hujenga utamaduni wa kuwajibika, kuimarisha nidhamu ya utumishi na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya umma, "alisema Jaji Mwangesi.

Alisema viongozi wenye maadili wanapotenda kwa haki, uwazi na uadilifu wanaongeza utiifu wa sheria na mshikamano na hivyo kuimarisha imani ya wananchi kwa serikali na taasisi zake 

"Maadili ni kinga ya maovu yote na nguzo muhimu ya utawala bora na maendeleo endelevu ya taifa" alisema Kamishna Mwangesi.

Kamishna huyo katika hotuba yake ya ufunguzi wa mafunzo ya maadili kwa viongozi wa umma iliyosomwa kwa niaba yake na Kamishna ofisi ya rais tume ya utumishi wa umma Nassor Mnambila, aliwataka viongozi kuwa mabalozi wa maadili kuanzia ngazi ya familia

Mafunzo hayo yanawashirikisha Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri na wakurugenzi wa serikali za mitaa. 

Mshiriki wa mafunzo hayo  Mstahiki Meya wa  Manispaa ya Tabora Gullam Dewji alisema viongozi wenye maadili siku zote wanatoa maamuzi yenye kuzingatia haki.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbeya Aidda Haule alisema mafunzo  kwa viongozi hao ni muhimu kwa nia ya kuimarisha Utawala bora.

"Serikali inapoleta miradi ya maendeleo kwa wananchi Halmashauri ndizo zinasimamia utekelezaji wa miradi yote hivyo ni lazima kuwepo na uadilifu katika usimamizi alisema Bi Haule.




Post a Comment

1 Comments

  1. Ningependa kumpendekeza mmoja wa wazimu wanaoheshimika zaidi wa wakati wetu. Ni mtu ambaye amewasaidia watu wengi jijini wakati wa hali ngumu.

    Baadhi ya watu hata humwita "mungu mdogo" kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kiroho na jinsi anavyowasaidia wale wanaomjia kwa ajili ya mwongozo.

    Unaweza kumtumia ujumbe kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe wightmagicmaster@gmail.com

    Tafadhali zungumza naye kwa heshima na ueleze hali yako wazi, naye atajitahidi kukusaidia.

    Anatoa mwongozo wa kiroho na usaidizi kwa hali tofauti, ikiwa ni pamoja na:

    • Masuala ya mapenzi na uhusiano, ikiwa ni pamoja na kusaidia kuungana tena na mpenzi wa zamani.

    • Kurejesha ndoa na mahusiano yenye matatizo.

    • Maombi na mila za kiroho kwa ajili ya ulinzi na mafanikio.

    • Tiba za mitishamba za kuponya VVU, saratani, malengelenge.

    • Maombi ya uzazi na usaidizi wa kiroho kwa wanandoa wanaotaka kupata mimba katika wiki chache.

    • Uwezo wa Telekinesis. Uwezo wa kubadilisha umbo.

    • Tambiko na maombi ya utajiri wa papo hapo.

    • Msaada wa kiroho katika hali ngumu kama vile kesi za mahakamani, kurejesha mali iliyopotea, na changamoto zingine za maisha.

    Watu wengi wamepokea msaada na mwongozo kupitia kazi yake ya kiroho.

    ReplyDelete



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI