Takriban watu 30 wamejeruhiwa kufuatia shambulizi la ndege zisizo na rubani za Urusi kwenye kituo cha reli kaskazini-mashariki mwa Ukraine, Rais wa Ukraine Volodymy Zelensky amesema.
Katika chapisho kwenye mtandao wa X, alisema kuwa ripoti za awali zilionyesha wafanyakazi wa treni na abiria walikuwa kwenye eneo la tukio katika jiji la Shostka, eneo la Sumy.
Huduma za dharura zinatolewa katika eneo la tukio na kusaidia watu, alisema na kuongeza kuwa taarifa kuhusu majeruhi bado zinakusanywa.
Pia alichapisha video inayoonyesha behewa la treni lililoharibika likiwaka moto.
0 Comments