Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, ametoa onyo kali kwa makundi au watu wenye nia ya kuanzisha fujo ama vurugu wakati wa kipindi cha uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo imara na makini kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kudumishwa nchini.
Malima ametoa kauli hiyo leo Jumatano Oktoba 22, 2025, wakati wa Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu, lililoandaliwa na Taasisi ya Ukumbusho wa Zakkat Tanzania na kufanyika mkoani Morogoro, akisema kuwa baadhi ya watu wanaojaribu kuvuruga amani nchini ni watu wanaoshawishiwa na kuiga matendo kutoka nje, na hawana nia njema na Taifa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Alhad Mussa , amesema watanzania wanapaswa kukataa kwa nguvu zote watu wanaoeneza chuki na kuhatarisha maisha ya wengine, hasa katika kipindi hiki nyeti cha uchaguzi.
0 Comments