Header Ads Widget

WAZIRI KOMBO AKUTANA NA BALOZI WA KENYA INCHINI TANZANIA ISAAC NJENGA



 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amekutana na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Isaac Njenga, katika jitihada za kuendelea kuimarisha ushirikiano na kuleta maendeleo kati ya nchi hizo mbili.

Wakati wa mazungumzo yao, Waziri Kombo amesisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania kuendeleza uhusiano wa muda mrefu na Kenya, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji, miundombinu na nishati, ili kukuza uchumi wa pamoja na kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa upande wake Balozi wa Kenya Mhe. Njenga amepongeza uhusiano mzuri uliopo baina ya mataifa haya mawili jirani na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza sekta za kipaumbele zinazochangia ustawi wa wananchi wa pande zote mbili.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI